Nchi 10 za Afrika zenye madeni ya kutisha 2026

Iliyochapishwa
Muda wa kusoma: Dakika 4

Viwango vya juu vya madeni vinavyodaiwa na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na wakopeshaji wengine wa nje vinaweza kusababisha hatari kubwa za kiuchumi za muda mrefu kwa nchi za Afrika, hasa kama uchumi unategemea kukopa isivyostahili ili kusawazisha fedha za umma au kusaidia uwekezaji muhimu kwa mujibu wa Business Insider Africa .

Ingawa mikopo ya IMF hutumiwa mara kwa mara ili kusaidia mataifa katika kudhibiti migogoro ya kiuchumi, mizigo ya muda mrefu ya madeni inaweza kudhoofisha matarajio ya maendeleo, kuzuia kubadilika kwa fedha, na kuongeza hatari ya majanga ya nje kama vile kupanda kwa bei ya mafuta, mfumuko wa bei duniani, au kupungua kwa mapato ya bidhaa.

Matukio ya hivi majuzi nchini Msumbiji, kama yalivyoonekana kwenye Reuters, na Angola yameangazia baadhi ya hatari hizi.

Msumbiji hivi karibuni imekabiliwa na uchunguzi unaoongezeka juu ya uhimilivu wa deni lake, huku kukiwa na wasiwasi kwamba hali ya kifedha ya nchi hiyo inazidi kuzorota zaidi.

Kulingana na Business Insider Africa, wachambuzi wa kimataifa na mashirika ya kukadiria wametahadharisha kuwa viwango vya deni vya Msumbiji vinazidi kuwa vigumu kushughulikia, na hivyo kuzua wasiwasi kwamba nchi hiyo hatimaye italazimika kujadili upya majukumu makubwa ya nje.

Masharti kama haya yanaweza kudhoofisha uaminifu wa wawekezaji, kupunguza ufikiaji wa masoko ya mitaji ya kimataifa, na kuongeza viwango vya kukopa kwa serikali na biashara.

Wakati nchi inachukuliwa kuwa haina utulivu wa kifedha, wawekezaji mara nyingi hudai viwango vya juu vya riba ili kufidia hatari.

Hii huongeza gharama ya ukopaji wa siku zijazo, kufungia uchumi katika mizunguko ambayo serikali hukopa hasa ili kuhudumia madeni yaliyopo badala ya kuendeleza sekta za uzalishaji kama vile viwanda, huduma za afya, miundombinu au elimu.

Kesi ya Angola, kama inavyoonekana kwenye Reuters, inaonyesha jinsi shinikizo la madeni linaweza kusalia hata katika uchumi tajiri wenye rasilimali.

Licha ya kunufaika na bei ya juu ya mafuta katika miezi ya hivi majuzi, nchi hiyo imepokea maonyo kwamba huenda deni lake la umma likafikia viwango hatari katika siku zijazo.

Hii inaangazia jinsi uchumi wenye madeni makubwa unavyoweza kutatizika kufikia uthabiti wa kifedha wa muda mrefu wakati vyanzo vyake vya mapato vinabadilika.

Pia inaonyesha kuwa wajibu wa madeni ya juu hupunguza uwezo wa serikali kujibu masuala muhimu katika uchumi.

Zifuatazo ni nchi za Afrika zenye madeni makubwa zaidi ya IMF mwaka huu .

1.Misri 7,245,182,524

2.Cote D'Ivoire. 3, 603,438 ,776

3.Kenya. 2, 873,418, 234

4.Ghana 2,728,468,500

5.Angola 2,437,716,676

6.DRC 2,196,550,004

7.Ethiopia 1,764,502,000

8.Tanzania. 1,335,730,000

9.Zambia 1,271,660,000

10.Cameroon. 1,152,990,000

Nchi 10 za Afrika zilizo na deni la chini zaidi kwa Shirika la IMF kufikia Aprili 2026

1. Namibia 0

2. Lesotho

3. Comoros

4.Djibout

5. Sao Tome na Principe

6. Guinea ya Equator

7.Guinea Bissau

8.Cabo Verde

9.Burundi

10. Syechelles