Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Moja kwa moja, Makubaliano ya kumaliza vita vya Iran 'yamejadiliwa kwa kiasi kikubwa' - Trump

Mpango wa kurefusha muda wa usitishaji mapigano umeripotiwa na vyombo vya Habari vya pande zote mbili lakini hakuna makubaliano rasmi yaliyofikiwa.

Muhtasari

Moja kwa moja

Na Ambia Hirsi

  1. Vita vya Iran: Starmer akaribisha wito wa makubaliano kuelekea kufunguliwa tena kwa Hormuz

    Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer amekaribisha "hatua iliyopigwa kuelekea makubaliano kati ya Marekani na Iran", na kuongeza kuwa ni "muhimu kwamba Iran kamwe isiruhusiwe kutengeneza silaha za nyuklia".

    Akiandika kwenye X asubuhi ya leo, muda mfupi baada ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio kuzungumza nchini India, Starmer alisema: "Tunarajia makubaliano ambayo yatamaliza mzozo na kufunguliwa tena kwa Mlango-Bahari wa Hormuz, kwa uhuru wa usafiri wa majini usio na masharti wala vikwazo."

    Starme alisema serikali ya Uingereza itafanya "kila tuwezalo" kuwalinda Waingereza kutokana na athari za vita, akiongeza kuwa atafanya kazi na washirika wa kimataifa "kutumia furasa hii kufikia suluhisho la muda mrefu la kidiplomasia".

    Soma zaidi:

  2. Rubio asema 'hatua kubwa' imepigwa katika mazungumzo ya Iran huku maelezo ya uwezekano wa makubaliano yakiibuka

    Waziri wa mambo ya nje wa Mavekani Marco Rubio aamesema "mafanikio makubwa" yamepatikana kwenye mpango wa kumaliza mzozo wa Iran, lakini "sio hatua ya mwisho"

    Alisisitiza msimamo wa Marekani kwamba "Iran kamwe haiwezi kumiliki silaha za nyuklia", akidai kwamba Donald Trump hatakubaliana na "upuuzi" huo.

    Alidokeza habari njema kwenye Mlango-Bahari wa Hormuz, akisema kwamba hatua imepigwa kueleke akufunguliwa tena kwa njia hiyo kuhimu ya majini katika muda wa saa 48 zilizopita - mpango huo ukifanya kazi - inaweza kusababisha hormuz "kutumika... bila ushuru."

    Rubio hata hivyo alisema bado kuna "kazi ya kufanya", akiongeza kuwa atamachia Trump kutoa matangazo zaidi.

    Huku hayo yakijiri Rais wa Tume ya Umoja wa Ulaya, Ursula von der Leyen, anasema anakaribisha "hatua iliyopigwa" katika mazungumzo ya Marekani na Iran, akiongeza kuwa "Iran lazima isiruhusiwe kutengeneza silaha za nyuklia".

    Amesema katika taarifa kwenye mtandao wa X kwamba mpango huo lazima "upunguze" mzozo na uhakikishe "usafiri huria bila malipo" katika Mlango-Bahari wa Hormuz.

    Von der Leyen ameongeza kuwa Iran lazima "ikomesha vitendo vyake vya kuyumbisha utulivu wa kikanda", moja kwa moja na kupitia washirika wake, na pia kukomesha "mashambulizi yake ya mara kwa mara" dhidi ya mataifa jirani ya Ghuba.

    "Ulaya itaendelea kufanya kazi na washirika wa kimataifa na kutumia wakati huu kwa suluhisho la kudumu la kidiplomasia," aliongeza.

    Soma zaidi:

  3. Mshukiwa auawa baada ya kuwafyatua risasi maafisa wa Secret Service karibu na Ikulu ya White House

    Mshukiwa aliyepiga risasi katika kituo cha ukaguzi cha Ikulu ameuawa katika makabiliano ya risasi na maafisa wa Secret Service Jumamosi jioni, maafisa wamethibitisha.

    CBS Mshirika wa BBC wa habari nchini Marekani imemtaja mshukiwa kuwa Nasire Best, mwanamume mwenye umri wa miaka 21 ambaye alikuwa anajulikana na shirika la ulinzi ambaye alikuwa anajulikana kuwa na historia hali ya afya ya akili.

    Rais wa Marekani Donald Trump aliwashukuru maafisa hao kwa "hatua yao ya haraka na ya kitaalamu" katika kumkamata mtu mwenye bunduki, ambaye alisema katika chapisho la kijamii wa Truth Social alikuwa na "historia ya vurugu na uwezekano wa kuzingatia muundo unaothaminiwa zaidi wa Nchi yetu".

    Tukio hilo la ufyatuaji risasi linakuja mwezi mmoja tu baada ya mtu mwenye silaha kufyatua risasi kwenye dhifa ya cha jioni cha Waandishi wa Habari wa White House.

    Tukio la Jumamosi bado linachunguzwa na barabara karibu na Ikulu ya White huenda ikaendelea kufungwa kwa usiku mmoja.

    Pia unaweza kusoma:

  4. Watu wanne wauawa katika wimbi la mashambulizi ya Urusi mjini Kyiv

    Watu wanne wameuawa na wengine zaidi ya 50 kujeruhiwa katika wimbi kubwa la mashambulizi ya makombora na ndege zisizo na rubani za Urusi mjini Kyiv na maeneo yanayoizunguka.

    Milipuko ilisikika mjini humo usiku wa kuamkia Jumapili.

    Meya wa Kyiv Vitali ⁠Klitschko alisema "ulikuwa usiku wa kutisha", na uharibifu uliripotiwa katika wilaya zote za mji mkuu, ikiwa ni pamoja na majengo ya makazi na shule.

    Watoto watatu ni miongoni mwa waliojeruhiwa, kazi ya uokoaji ikiendelea.

    Mashambulizi hayo yanafuatia tishio la Rais wa Urusi Vladimir Putin cha kulipiza kisasi baada ya kuishutumu Ukraine kwa kutekeleza shambulio baya kwenye bweni la wanafunzi katika mji wa Starobilsk siku ya Ijumaa ambapo watu 18 waliuawa.

    Wafanyakazi wa jumla wa vikosi vya jeshi vya Ukraine walisema walifanya shambulizi karibu na Starobilsk mashariki mwa Ukraine inayokaliwa na Urusi usiku wa kuamkia leo, lakini walishikilia kuwa walishambulia kitengo cha kijeshi cha Urusi.

    Mashambulizi ya usiku ya Urusi siku ya Jumapili yalikuja baada ya Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky kuonya kuwa kuna dalili kwamba Urusi inatayarisha "mgomo wa pamoja katika ardhi ya Ukraine".

    Alitoa mfano wa kijasusi kutoka Ukraine, Ulaya na Marekani kupendekeza Urusi inaweza kuwa na mpango wa kutumia kombora la Oreshnik, ambalo linaripotiwa kusafiri zaidi ya mara 10 ya kasi ya sauti na kwa sasa haliwezekani kulinasa.

    Bado haijathibitisha ikiwa Urusi ilitumia kombora katika shambulio lake la hivi punde.

    Soma zaidi:

  5. Mlango wa bahari wa Hormuz 'hautarejea' ulivyokuwa kabla ya vita - vyombo vya habari vya Iran

    Chini ya makubaliano kati ya Marekani na Iran, Mlango wa bahari wa Hormuz "hautarejea katika hali yake ya kabla ya vita" linaripoti shirika la habari la Iran la Tasnim.

    Chombo hicho cha habari kilicho na uhusiano na Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) kimekuwa kikiripoti maelezo yaliyomo kwenye makubaliano hayo na Marekani asubuhi hii, lakini Marekani haijathibitisha kuhusu maelezo ya makubaliano yoyote.

    Tasnim inaripoti kwamba mlango huo wa bahari hautarudi katika "ilivyokuwa" lakini idadi ya meli zinazopita inaweza kurudi katika viwango vya kabla ya vita ndani ya siku 30.

    Hata hivyo, inaongeza kuwa Iran "inasisitiza kutumia mamlaka yake kuhusu uamuzi huo".

    Inaongeza kuwa kizuizi cha majini cha Marekani dhidi ya meli zinazoingia na kutoka bandari za Iran lazima "kiondolewa kabisa" ndani ya siku 30.

    Maelezo zaidi:

  6. Makubaliano ya kumaliza vita vya Iran 'yamejadiliwa kwa kiasi kikubwa' - Trump

    Rais wa Marekani Donald Trump anasema makubaliano ya kumaliza vita vya Iran "yamejadiliwa kwa kiasi kikubwa" na maelezo yatatangazwa hivi karibuni.

    Katika chapisho kwenye mtandao wake wa kijamii wa Truth Socialsiku ya Jumamosi, Trump alisema makubaliano hayo yatajumuisha kufunguliwa tena kwa Mlango-Bahari wa Hormuz.

    Asubuhi ya leo, shirika la habari la Iran la Tasnim limesema kuwa Mlango wa Bahari utarejea katika viwango vya kabla ya vita ndani ya siku 30, na kuongeza kuwa makubaliano huenda yakasimamisha mashambulizi pande zote.

    Muda mfupi ujao tunatarajia tamko kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio kufuatia mkutano wake na waziri wa mambo ya nje wa India mjini New Delhi - unaweza kufuatilia moja kwa moja hapo juu pindi atakapoanza.

    Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Iran Esmail Baghaei aliambia televisheni ya taifa jana kuwa wawakilishi wa Marekani na Iran wamekuwa wakikutana katika wiki za hivi karibuni.

    Lakini alionya hilol haimaanishi kuwa makubaliano yatafikiwa katika masuala muhimu na kuwashutumu Wamarekani kwa kutoa "taarifa zinazokinzana".

    Trump pia alisema alikuwa na "mazungumzo mazuri" na viongozi wa Saudi Arabia, Umoja wa Falme za Kiarabu, Qatar, na wengine kuhusu "Mkataba wa Maelewano unaohusu AMANI".

    Maelezo zaidi:

  7. Karibu kwa matangazo ya moja kwa moja.