Ndege za kivita za Uingereza zazuia ndege ya kijeshi ya Urusi
Ndege za kivita za Uingereza zimeizuia ndege ya doria ya Urusi baada ya kuikaribia meli ya kivita katika Bahari ya Norway, imesema Wizara ya Ulinzi (MoD).
Ndege ya Urusi aina ya Bear-F ilipita "karibu sana" na meli ya kubeba ndege za kivita ya HMS Prince of Wales na inaaminika kuwa ilidondosha mabiya 10 ya kufuatilia nyambizi ndani ya maji siku ya Alhamisi, Wizara ya Ulinzi iliongeza.
Wizara ya Ulinzi imesema shughuli za Moscow katika Bahari ya Norway "si salama na zisizo za sawa".
Hii inakuja wiki kadhaa baada ya wanajeshi wa Royal Marines kupanda meli ya mafuta ya Urusi katika Mlango wa Uingereza, huku mkuu wa jeshi akionya kwamba hatari na vitisho vinavyoikabili Uingereza ni vikubwa zaidi sasa kuliko wakati mwingine wowote tangu Vita Baridi.
Meli za kivita za Uingereza kwa sasa zimetumwa nje ya Iceland chini ya amri ya Nato, zikiwa na wanajeshi 1,500 wa Uingereza ndani.
Kundi hilo linajumuisha manowari ya HMS Prince of Wales, manowari ya HMS Duncan, ndege aina ya F-35, helikopta za Merlin na Wildcat, na manowari ya RFA Tidespring ya kujaza mafuta.
Ni mara ya kwanza kwa Nato kufanya operesheni za ulinzi wa anga kutoka meli ya kivita ya Ulaya.
Pia unaweza kusoma: