Tetesi za soka Ulaya Jumanne: Arsenal yamtaka mchezaji wa DRC Congo Aaron Wan Bissaka

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Aaron Wan Bissaka
Iliyochapishwa
Muda wa kusoma: Dakika 2

Arsenal imemwongeza beki wa kulia wa West Ham na DR Congo Aaron Wan-Bissaka, 28, kwenye orodha yao ya wachezaji wanaoweza kuchukua nafasi ya Ben White, iwapo mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza ataondoka msimu huu wa joto. (Teamtalk)

Tottenham itajaribu kumnunua mshambuliaji wa Bournemouth na Ufaransa Eli Junior Kroupi kwa dau la pauni milioni 85 , licha ya Cherries kusisitiza kwamba mchezaji huyo wa miaka 20 hauzwi. (Talksport)

Atletico Madrid itatafuta kujaza nafasi ya Antoine Griezmann na nyota wa zamani wa Liverpool Mohammed Salah, 33, ambaye kwa sasa yuko kwenye Kombe la Dunia na Misri. (Fichajes - In Spanish )

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Mohammed Salah

Liverpool wamejiunga na Chelsea na Manchester United katika kinyang'anyiro cha kumsajili mshambuliaji wa West Ham, Mholanzi, Crysencio Summerville, 24. (Caught Offside)

Moja ya kazi za awali za Andoni Iraola kama kocha wa Liverpool itakuwa ni kusimamisha nia ya kutaka kusajiliwa na Old Trafford na Ulaya ili kumsajili kiungo wa kimataifa wa Mexico mwenye umri wa miaka 17, Gilberto Mora, ambaye anacheza soka lake la ndani kwa Klabu ya Tijuana. (Teamtalk)

Chelsea itampa mkataba mpya mchezaji wa kimataifa wa Uingereza chini ya miaka 19, Jesse Derry, 19, ili kusimamisha nia ya kusajiliwa na Bayern Munich. (Football Insider,)

.

Chanzo cha picha, Real Madrid

Maelezo ya picha, Dani Carvajal

Wolves wana nia ya kumsajili kiungo wa kati Niko Sigur, 22, kutoka Hadjuk Split baada ya kuchezea Kombe la Dunia kwa Kroatia. (Sky Sports,)

Mchezaji wa kimataifa wa Uhispania Dani Carvajal, 34, anaweza kujiunga na Deportivo La Coruna aliyepanda daraja hivi karibuni baada ya kuondoka Real Madrid. (Fichajes - In Spanish)