Moja kwa moja, Hezbollah yakubali kusitisha mashambulizi dhidi ya Israel - Lebanon

Ubalozi wa Lebanon nchini Marekani ulisema "umepokea uthibitisho wa kukubali kwa Hezbollah pendekezo la Marekani la kukomesha mashambulizi kwa pande zote mbili".

Muhtasari

Moja kwa moja

Na Asha Juma

  1. Rais wa Senegal atangaza baraza jipya la mawaziri

    Rais wa Senegal Rais Bassirou Diomaye Faye ametangaza baraza jipya la mawaziri lenye wajumbe 30. Hatua hiyo imekuja wiki moja baada ya kuteuliwa kwa mwanauchumi Ahmadou Al Aminou Mohamed Lo kuwa Waziri Mkuu.

    Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na chama cha PASTEF kabla ya tangazo hilo, hakukuwa na mwanachama yeyote wa chama cha Ousmane Sonko ambaye alipaswa kujumuishwa katika baraza hilo jipya la mawaziri.

    "PASTEF inatangaza kwamba haitashiriki katika serikali ijayo. Chama hicho kinataja kuwepo kwa tofauti kubwa kuhusu nafasi na jukumu la walio wengi katika mpangilio wa mamlaka ya utendaj," Taarifa hiyo ilisema.

    Hata hivyo, baadhi ya wanachama wa PASTEF hatimaye walirejeshwa serikalini, akiwemo Dkt. Alioune Dione, Waziri wa Fedha na Uchumi na Waziri wa Afya Ibrahima Sy.

    Tangazo la serikali hilo la Juni Mosi, linaonekana kuwa mchanganyiko wa mwendelezo na mabadiliko, huku mawaziri kadhaa wakihifadhi nyadhifa zao kutoka serikali ya Sonko na wakati huo huo viongozi wa zamani wenye uzoefu wakirejea katika uongozi.

    Senegal inapitia misukosuko ya kisiasa huku wanasiasa wake wawili maarufu zaidi – Rais Bassirou Diomaye Faye na Spika Ousmane Sonko – wakijihusisha katika mvutano mkubwa wa kisiasa.

    Ousmane Sonko, ambaye alikuwa Waziri Mkuu, aliondolewa katika wadhifa huo siku kumi zilizopita kisha akachaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Taifa la Senegal.

    Wadhifa wa Sonko, ambaye alikuwa Waziri Mkuu kuanzia Aprili mwaka 2024 hadi Mei 2026 ulichukuliwa na Ahmadou Al Aminou Mohamed Lo, Mwana Uchumi mwenye umri wa miaka 60, aliyekuwa afisa wa Benki ya Afrika Magharibi.

  2. Ruto atetea kituo cha Ebola kilichoombwa na Marekani kujengwa Kenya

    .

    Chanzo cha picha, State House Kenya/Facebook

    Rais William Ruto ametetea mradi wa ujenzi wa kituo cha Ebola kilichoombwa na Marekani huko Laikipia, akiondoa wasiwasi kuhusu mradi huo na kusisitiza kuwa unalenga kuimarisha utayari wa Kenya kukabiliana na ugonjwa wa Ebola.

    Akiongea wakati wa mahojiano na vyombo vya habari katika sherehe za sikukuu ya Madaraka Juni 1, Rais Ruto alithibitisha kwamba aliidhinisha mrada huo binafsi baada ya ombi kutoka kwa Rais Donald Trump, akiutaja kama sehemu ya ushirikiano wa muda mrefu kati ya nchi hizo mbili.

    "Rais Trump alipoomba serikali ya Kenya iwaunge mkono kwa kuwa na kituo cha kukabiliana na Ebola katika kambi ya jeshi la anga ya Laikipia, nilikubali kwa sababu ilikuwa makubaliano na ushirikiano na marafiki ambao wameshirikiana na Kenya," alisema Rais Ruto.

    "Kwa miaka 30, 40, serikali ya Marekani imetuunga mkono. Wametumia rasilimali nyingi nchini Kenya kushirikiana nasi katika VVU, UKIMWI, na magonjwa mengine."

    Alisisitiza kuwa kituo hicho hakina tofauti na vingine 23 vya maandalizi ya Ebola ambavyo tayari vipo kote nchini.

    Rais alisema vituo kama hivyo vipo katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta, Hospitali ya Polisi jijini Nairobi, Hospitali ya Mafunzo na Rufaa ya Moi huko Eldoret, na Hospitali ya Alupe huko Busia.

    Rais Ruto alisisitiza kwamba Kenya huwachunguza takriban wasafiri 3,000 kila siku katika vituo vyote vya kuingia nchini, na hakuna kisa chochote cha Ebola kilichorekodiwa kufikia sasa.

    Aliongeza kuwa mipaka ya ardhini na angani inasalia kuwa katika tahadhari kubwa, na itifaki za karantini na kutengwa tayari zimewekwa kote nchini.

    Pia unaweza kusoma:

  3. Awaua wanafamilia sita kabla ya kujiua mwenyewe, polisi wanasema

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Mwanafamilia aliyekuwa na bunduki amewaua watu sita wa familia yake, kisha akajiua, katika shambulizi lililohusisha mfululizo wa ufyatuaji risasi siku ya Jumatatu katika jiji la Muscatine mashariki mwa Iowa, mji ulioko ufukweni mwa mto Mississippi kutoka Illinois, polisi wamesema.

    Uchunguzi wa awali kuhusu vurugu za bunduki ulionyesha kuwa ufyatuaji risasi "ulitokana na mzozo wa ndani," Idara ya Polisi ya Muscatine ilisema katika taarifa, ingawa hakuna kilichotajwa haswa kuhusu kile ambacho huenda kilisababisha umwagaji damu.

    Wanne kati ya waathiriwa walipatikana wakiwa wamepigwa risasi hadi kufa ndani ya makazi kulingsna na maafisa wa polisi wakijibu ripoti za kwanza za milio ya risasi muda mfupi baada ya saa sita mchana kwa saa za eneo.

    Ingawa mshukiwa wa muuaji alikuwa ametoroka eneo la tukio kabla ya maafisa kufika, alitambuliwa haraka kama Ryan Willis McFarland, 52, wa Muscatine, na alikuwa kwenye njia ya mji karibu na daraja la watembea kwa miguu, Mkuu wa Polisi Anthony Kies alisema wakati wa mkutano na waandishi wa habari.

    Wakati maafisa walipokuwa wakizungumza naye, alijiua, polisi walisema.

    Baada ya taarifa kuibuka zikionyesha kuwa huenda kulikuwa na waathiriwa wengine, polisi walipata miili ya watu wengine wawili ambao McFarland aliaminika kuwapiga risasi - mmoja katika nyumba iliyo karibu na mwingine katika biashara.

    Waathiriwa wote waliaminika kuwa wanafamilia wa mshambuliaji huyo, Kies alisema. Hawakutambuliwa hadharani na inasemekana kuwa takriban wawili kati ya waathiriwa walikuwa watoto.

    Mkuu wa polisi aliwaambia waandishi wa habari kwamba McFarland alikuwa na rekodi ya uhalifu hapo awali lakini alikataa kufafanua.

    Soma zaidi:

  4. Mashambulizi makubwa ya Urusi yaikumba Ukraine usiku kucha

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Watu watano wameuawa na makumi kadhaa kujeruhiwa nchini Ukraine baada ya Urusi kuanzisha shambulio kubwa usiku kucha.

    Watu wanne wameuawa huko Dnipro na 16 wamejeruhiwa. Mtu mmoja pia aliuawa huko Kyiv, huku wengine takriban 20 wakijeruhiwa kufuatia mashambulizi ya Urusi mapema Jumanne.

    Maelfu ya watu walikimbilia mji wa Kyiv huku moshi mwingi ukipanda kutoka katikati ya jiji. Maonyo ya uvamizi wa anga yalikuwa yamewekwa katika sehemu kubwa ya Ukraine.

    Meya wa Kyiv Vitali Klitschko amewasihi watu kukaa majumbani mwao. Mkuu wa Utawala wa Jeshi la Jiji la Kyiv, Tymur Tkachenko, alisema: "Adui anashambulia kwa makombora ya balestiki".

    Klitschko alisema majengo mawili marefu ya ghorofa yameathiriwa na kuna hofu kwamba watu wamenaswa chini ya vifusi.

    Huku mashambulizi ya Urusi yakiikumba Kyiv hadi asubuhi na mapema, mlio wa ndege zisizo na rubani ilisikika kati ya milipuko mikubwa zaidi kumi na miwili huku mashambulizi yakiendelea.

    Kukatika kwa meme na matukio ya moto pia kumeripotiwa kote jijini na ukubwa wa uharibifu bado hakujabainika.

    Kituo cha viwanda pia kimeshambuliwa huko Zaporizhzhia.

    Soma zaidi:

  5. Hezbollah yakubali kusitisha mashambulizi dhidi ya Israel - Lebanon

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Lebanon inasema Hezbollah imekubali mpango wa Marekani wa kusimamisha mashambulizi dhidi ya Israel na Israel isiushambulie mji mkuu wa Lebanon Beirut.

    Ubalozi wa Lebanon nchini Marekani ulisema "umepokea uthibitisho wa kukubali kwa Hezbollah pendekezo la Marekani la kukomesha mashambulizi kwa pande zote mbili".

    Waziri Mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu alithibitisha makubaliano hayo, lakini alionya kwamba mashambulizi dhidi ya Beirut yataendelea "ikiwa Hezbollah haitaacha kushambulia miji yetu na raia".

    Taarifa hizo zilikuja baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kusema amezungumza na wawakilishi wa Netanyahu na Hezbollah na "walikubaliana kwamba ufyatuaji risasi wote utakoma", baada ya Iran kuonya kwamba vitendo vya kijeshi vya Israeli nchini Lebanon ni tishio kwa usitishaji mapigano wa sasa kati ya Marekani na Iran.

    Katika taarifa iliyotolewa Jumatatu jioni, ubalozi wa Lebanon ulisema kwamba "chini ya mpango uliopendekezwa, mashambulizi ya Israeli kwenye vitongoji vya kusini mwa Beirut yatakoma badala ya Hezbollah kujizuia na mashambulizi dhidi ya Israeli". Iliongeza kuwa usitishaji mapigano "utaongezwa ili kujumuisha eneo lote la Lebanon".

    Hata hivyo Netanyahu alisema: "Wakati huo huo, IDF [Vikosi vya Ulinzi vya Israeli] itaendelea kuendesha shughuli zake kusini mwa Lebanon kama ilivyopangwa."

    Baada ya Trump kusema pande zote mbili zimekubaliana kuacha kupigana, mapigano mengine yaliendelea.

    Hezbollah ilisema imeanzisha mashambulizi matatu dhidi ya vifaru na wanajeshi wa Israeli karibu na vijiji viwili kaskazini mwa Israeli, ikitumia ndege zisizo na rubani na "makombora ya mizinga".

    Soma zaidi:

  6. Karibu katika matangazo yetu mubashara ya terehe 02/06/2026.