Brazil inawafuatilia wagonjwa wawili kwa uwezekano wa kuambukizwa Ebola

Chanzo cha picha, Getty Images
Maafisa wa afya nchini Brazil wamesema wanachunguza kisa cha pili kinachoshukiwa kuwa cha Ebola mjini Rio de Janeiro ambapo raia wa Ubelgiji hivi karibuni aliwasili kutoka Uganda.
Raia huyo alionyesha"dalili za virusi kama vile kikohozi, baridi na kuhara".
Kisa kingine kinachoshukiwa kiligunduliwa Jumamosi katika jimbo la São Paulo. Matokeo ya vipimo kwa wagonjwa wote wawili yanatarajiwa kupatikana wiki ijayo.
Iwapo yatathibitishwa, hii itakuwa mara ya kwanza kwa maambukizi hayo kuripotiwa nje ya Afrika tangu mlipuko ulipoanza nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.
Mlipuko wa sasa kuna zaidi ya maambukizi 1,000 yenye kushukiwa kuwa Ebola nchini DR Congo, huku vifo vikishukiwa kuwa takriban 246. Uganda imeripoti maambukizi tisa yaliothibitishwa na kifo kimoja.
Mlipuko wa sasa umesababishwa na aina adimu ya Ebola inayojulikana kama Bundibugyo, ambayo haina chanjo iliyothibitishwa.
Awali, mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Tedros Adhanom Ghebreyesus aliwataka watu nchini DRC kutafuta matibabu haraka iwapo watahisi dalili za ugonjwa huo.
Soma zaidi:




