Tetesi za soka Ulaya Ijumaa: Inter Milan wanasuka mipango kumsajili Spence

Chanzo cha picha, Getty Images
Inter Milan wanania ya kumsajili Djed Spence na Cristian Romero, Liverpool wanaongoza mbio za kumsajili Kaishu Sano, huku Arsenal wakimwania Ezri Konsa.
Inter Milan wanasuka mipango ya kumsajili beki wa pembeni wa Tottenham na England, Djed Spence, 25, pamoja na beki wa kati wa Argentina, Cristian Romero, 28. (Corriere dello Sport - in Italian)

Chanzo cha picha, Getty Images
Liverpool wanaongoza mbio za kumsajili kiungo wa Japan, Kaishu Sano, kutoka Mainz na wako tayari kutoa hadi euro milioni 60 (£50.9m) kwa ajili ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, ambaye pia anawindwa na Arsenal, Tottenham na Borussia Dortmund. (Teamtalk)

Chanzo cha picha, Getty Images
Arsenal wameonyesha nia ya kumsajili beki wa Aston Villa na England, Ezri Konsa, mwenye umri wa miaka 28. (Guardian)

Chanzo cha picha, Getty Images
Kipa wa Crystal Palace na Argentina, Walter Benitez, mwenye umri wa miaka 33, anaweza kuvunja mkataba wake na Palace ili kurejea Nice. (Nice-Matin - in French)
Liverpool wamewasiliana na Bournemouth kuhusu winga wa miaka 19, Rayan, wakilenga kumrejesha Mbrazil huyo chini ya kocha wao wa zamani, Andoni Iraola. (Teamtalk)

Chanzo cha picha, Getty Images
Newcastle wanaendelea na mazungumzo ya kumsajili kipa wa Brighton, Carl Rushworth, 25, na Mwingereza mwenzake James Trafford, mlinda lango wa Manchester City mwenye umri wa miaka 23. (Mail - requires subscription)
Fulham wamekuwa kama Coventry na Chelsea kumfuatilia winga wa Strasbourg na Ivory Coast Martial Godo, 23. (Africafoot - in French)

Chanzo cha picha, Getty Images
Ipswich wamewasilisha ofa ya kumsajili winga wa Leicester na Ghana, Abdul Fatawu, mwenye umri wa miaka 22. (Telegraph)

Chanzo cha picha, Getty Images
Leeds wanaendelea na harakati zao za kumsaka kipa wa Parma na Japan Zion Suzuki, 23, licha ya klabu ya Italia kutokuwa tayari kumruhusu aondoke. (Tuttomercatoweb - in Italian)
Crystal Palace wana nia ya kumsajili beki wa Augsburg Chrislain Matsima, 24, huku Mfaransa huyo akiwa mmoja wa chaguo la mabeki wa kati wanaofuatiliwa. (Standard)














