Iran ilipe fidia kwa madhara iliyosababisha wakati wa vita - Trump
Rais wa Marekani Donald Trump amesema Iran inapaswa kulipa fidia kwa watu walioathiriwa na vifo na majeraha yaliyosababishwa na matukio mbalimbali katika kipindi cha miaka 50 iliyopita.
Trump amesema kauli hiyo inajibu madai ya Iran ya kutaka kulipwa fidia kwa uharibifu unaodaiwa kusababishwa na Marekani.
“Waliomba fidia, unaweza kusema, au waliomba fedha kwa ajili ya uharibifu ambao tumesababisha. Nikasema hilo ni wazo zuri. Basi nasi tutaomba fedha kwa ajili ya uharibifu ambao wao wamesababisha kwa kipindi cha miaka 50,” Trump amesema.
Ametaja pia shambulio la meli ya kijeshi ya Marekani USS Cole na watu waliouawa au kujeruhiwa katika matukio mbalimbali.
Trump pia amesema familia za watu waliouawa katika maandamano nchini Iran zinapaswa kulipwa fidia.
“Tunafikiri familia zao zinapaswa kupata fidia kwa kuuawa kwa mtu wao, mtoto wao, mama au baba yao waliokuwa wakiandamana,” Trump amesema.
Amedai kuwa watu 52,000 waliuawa katika maandamano nchini Iran katika kipindi cha miezi minne iliyopita, ingawa kauli hiyo BBC haijathibitisha kwa uhuru.
Trump amesema iwapo fidia italipwa, Iran ndiyo inapaswa kubeba gharama hiyo.
Soma Zaidi Hapa: