Trump asema atamjibu Netanyahu kuhusu mpango wa amani wa Gaza

Chanzo cha picha, Getty Images
Rais wa Marekani Donald Trump amesema hivi karibuni atajibu kauli ya Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ya kuukataa mpango wa amani wenye vipengele 15 wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Trump, akijibu maswali ya waandishi wa habari ndani ya Ikulu ya Marekani, amesema atachapisha majibu yake kwenye mtandao wake wa kijamii wa Truth Social.
“Nitachapisha jibu langu huko. Nina jibu, ni jibu zuri, nitalichapisha huko,” Trump amesema.
Amesema pia uhusiano wake na Netanyahu bado ni “mzuri sana.”
Katika siku za hivi karibuni, kumekuwa na kusitishwa kwa mashambulizi ya Israel dhidi ya Gaza, angalau kwa kiwango fulani, jambo ambalo Hamas ililitaka wakati ilipokubali mpango wa vipengele 15 unaoungwa mkono na Marekani.
Pia kuna dalili nyingine kwamba Israel iko tayari kuendeleza mpango wa amani wa Rais wa Marekani Donald Trump kwa Gaza, ikiwa ni pamoja na maandalizi ya kupelekwa kwa Kikosi cha Kimataifa cha Kuleta Utulivu (ISF). Kikosi hicho kinaundwa na wanajeshi kutoka nchi mbalimbali, na mpango ni kwamba watashirikiana na kikosi kipya cha polisi wa Palestina katika kuhakikisha usalama wa eneo hilo.
Ujenzi wa kituo cha kwanza cha ISF bado unatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi huu, miongoni mwa magofu ya Rafah, kusini mwa Gaza, kwa mujibu wa redio ya umma ya Israel, Kan News. Hatua hiyo itawezesha hatimaye kuanza kwa ujenzi upya wa eneo hilo.
Soma Zaidi Hapa:


