Moja kwa moja, Trump asema Marekani imeondoa mabomu ya baharini katika Mlango wa Hormuz

Rais wa Marekani Donald Trump amesema Jeshi la Wanamaji la Marekani ndilo linalodhibiti kwa sasa Mlango wa Hormuz.

Muhtasari

Trump asema Marekani imeondoa mabomu ya baharini katika Mlango bahari wa Hormuz

Moja kwa moja

Na Mariam Mjahid

  1. Trump asema atamjibu Netanyahu kuhusu mpango wa amani wa Gaza

    d

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Rais wa Marekani Donald Trump amesema hivi karibuni atajibu kauli ya Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ya kuukataa mpango wa amani wenye vipengele 15 wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

    Trump, akijibu maswali ya waandishi wa habari ndani ya Ikulu ya Marekani, amesema atachapisha majibu yake kwenye mtandao wake wa kijamii wa Truth Social.

    “Nitachapisha jibu langu huko. Nina jibu, ni jibu zuri, nitalichapisha huko,” Trump amesema.

    Amesema pia uhusiano wake na Netanyahu bado ni “mzuri sana.”

    Katika siku za hivi karibuni, kumekuwa na kusitishwa kwa mashambulizi ya Israel dhidi ya Gaza, angalau kwa kiwango fulani, jambo ambalo Hamas ililitaka wakati ilipokubali mpango wa vipengele 15 unaoungwa mkono na Marekani.

    Pia kuna dalili nyingine kwamba Israel iko tayari kuendeleza mpango wa amani wa Rais wa Marekani Donald Trump kwa Gaza, ikiwa ni pamoja na maandalizi ya kupelekwa kwa Kikosi cha Kimataifa cha Kuleta Utulivu (ISF). Kikosi hicho kinaundwa na wanajeshi kutoka nchi mbalimbali, na mpango ni kwamba watashirikiana na kikosi kipya cha polisi wa Palestina katika kuhakikisha usalama wa eneo hilo.

    Ujenzi wa kituo cha kwanza cha ISF bado unatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi huu, miongoni mwa magofu ya Rafah, kusini mwa Gaza, kwa mujibu wa redio ya umma ya Israel, Kan News. Hatua hiyo itawezesha hatimaye kuanza kwa ujenzi upya wa eneo hilo.

    Soma Zaidi Hapa:

  2. Wahouthi washambulia mji wa Mukha nchini Yemen

    S

    Chanzo cha picha, EPA

    Vikosi vinavyoiunga mkono serikali ya Yemen vimesema wapiganaji wa Houthi wameushambulia mji wa bandari wa Mukha.

    Katika taarifa iliyochapishwa kwenye ukurasa wa jeshi la Yemen kwenye mtandao wa X, jeshi hilo limesema Wahouthi walifyatua makombora ya balistiki kuelekea mji huo uliopo katika pwani ya Bahari ya Shamu.

    Jeshi hilo pia limesema maeneo na vituo kadhaa katika bandari ya Mukha vililengwa katika mashambulizi hayo.

    Pia Unaweza kusoma:

  3. Trump asema Marekani imeondoa mabomu ya baharini katika Mlango wa Hormuz

    D

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Rais wa Marekani Donald Trump amesema vikosi vya Marekani vimeondoa mabomu ya baharini katika Mlango wa Hormuz na kuifanya njia hiyo kuwa salama kwa usafiri wa meli.

    Trump amesema Jeshi la Wanamaji la Marekani ndilo linalodhibiti kwa sasa Mlango wa Hormuz.

    “Angalia, kwa sasa ni Jeshi la Wanamaji la Marekani pekee ndilo linalodhibiti Mlango wa Hormuz,” aliwaambia waandishi wa habari katika Ofisi ya Oval ya Ikulu ya Marekani.

    Aidha Trump amesema Marekani imeweka kizuizi imara katika njia hiyo na inaruhusu kupita meli ambazo inataka.

    “Tumeweka kizuizi kinachofanya kazi kikamilifu na kisichoweza kupenywa, kama ukuta wa chuma.”

    Trump pia amesema baadhi ya mabomu ya baharini huwekwa katika njia hiyo, lakini vikosi vya Marekani huyagundua na kuyaondoa.

    “Ni jambo gumu kidogo, bila shaka, kwa sababu wakati mwingine wanaweka mabomu ya baharini, lakini sisi tunayagundua. Unajua, tumeondoa mabomu mangapi katika njia hii yote ya majini,” Trump alisema.

    Soma Zaidi Hapa:

  4. Hujambo na karibu kwa matangazo ya moja kwa moja ya tarehe 11/08/2026.