Lissu alivyoanza kumuhoji shahidi
Baada ya Mahamba kumaliza ushahidi wake wa msingi, Lissu alianza kumuhoji katika hatua ya cross-examination.
Lissu alimuuliza kama anajiona kuwa afisa mpelelezi mwenye uzoefu mkubwa.
Shahidi: "Ni kweli."
Lissu kisha akamuuliza kama alipanda cheo kwa kutungia watu kesi za uongo, kutesa watuhumiwa au kukosa uadilifu.
Shahidi: "Sio kweli."
Lissu pia alidai kuwa shahidi na timu yake walishirikiana na wahalifu waliofanya vurugu katika uchaguzi wa mwaka jana.
Shahidi: "Sio kweli."
Lissu aibua tofauti kati ya ushahidi na maelezo ya shahidi
Lissu alimwomba shahidi kueleza kama baadhi ya taarifa alizozitoa mahakamani zilikuwepo kwenye maelezo yake ya awali.
Katika maswali kadhaa, shahidi alijibu:
"Hayapo."
Miongoni mwa mambo hayo ni maelezo kuhusu mafunzo yake ya polisi, kituo chake cha kwanza cha kazi, mafunzo maalumu aliyodai kuyapata mwaka 2006, kuwa mkufunzi na baadhi ya majukumu aliyowahi kufanya.
Maelezo ya shahidi yapokelewa kama kielelezo D15
Baada ya mabishano mafupi kati ya Lissu na upande wa mashtaka kuhusu utaratibu wa kutumia maelezo hayo, mahakama iliruhusu yaendelee kutumika.
Maelezo hayo yalipokelewa na mahakama kama kielelezo D15.
Baadaye Jaji Dunstan Ndunguru aliahirisha kesi hadi leo saa tatu asubuhi.
Kesi inaendelea leo na Lissu anatarajiwa kuendelea kumuhoji shahidi katika hatua ya kumuuliza maswali shahidi kupima uamini na kuonyesha migongano (cross-examination)

