Araqchi: Uwezekano wa kurejea kwenye mkondo wa diplomasia ungalipo
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anasema uwezekano wa "kurejea katika mazungumzo ya kidiplomasia upo, lakini Marekani inastahili kuelewa kwamba kutumia nguvu hakufanyi kazi."
Katika ujumbe kwenye mtandao wa kijamii wa X, Abbas Araqchi alielezea mazungumzo yake na Mohammed bin Abdulrahman Al Thani, Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar, kuwa yenye "tija," na kusema: "Shinikizo halifanyi kazi.
Marekani lazima ijenge imani, izungumze kwa heshima, itambue haki za Iran, na itimize ahadi zake."
Waziri Mkuu wa Qatar alisafiri hadi Tehran jana akiongoza ujumbe, ambapo alikutana na kufanya mazungumzo na maafisa wa ngazi ya juu, akiwemo Masoud Pezeshkian na Mohammad Baqer Qalibaf, Rais na Spika wa Bunge la Iran.
Taarifa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar ilisema kuwa mkutano huo ulijadili "hali ya hivi karibuni katika eneo hilo" na "kuandaa mazingira mwafaka ya mazungumzo yatakayosaidia kuimarisha usalama na utulivu katika eneo hilo."
Maelezo zaidi: