Moja kwa moja, Marekani yaishambulia Iran, licha nya makubaliano kuwa karibu kuafikiwa

Majeshi ya Marekani yamesema yamedungua ndege kadhaa zisizo na rubani za Iran zilizokuwa zikielekea katika Mlango bahari wa Hormuz, wakati ambapo Washington na Tehran zimeashiria kuwa karibu kuafikia makubaliano ya kumaliza vita.

Moja kwa moja

Na Beldeen Waliaula

  1. Marekani yaichapa Paraguay 4-1, kufanya maajabu mwaka huu?

    us

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Marekani imeanza vyema kampeni yake ya Kombe la Dunia 2026 baada ya kuichapa Paraguay mabao 4-1 mjini Los Angeles na kuongoza Kundi D.

    Nyota wa zamani wa Arsenal, Folarin Balogun, alifunga mabao mawili katika ushindi huo mkubwa wa wenyeji wenza wa mashindano hayo.

    Katika mchezo mwingine, mwenyeji mwingine Canada ililazimishwa sare ya mabao 1-1 dhidi ya Bosnia-Herzegovina na kujikusanyia alama moja katika mechi yake ya kwanza ya kundi.

    Nayo Mexico ilianza kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Afrika Kusini, ikiweka wazi dhamira yake ya kufanya vizuri mbele ya mashabiki wake.

    Hadi sasa, mataifa yote matatu yanayoandaa Kombe la Dunia 2026 yamecheza mechi zao za ufunguzi, huku Mexico na Marekani zikianza kwa ushindi na Canada ikipata sare. Zitafanya maajabu mwaka huu?

  2. Marekani yamfukuza mwanaharakati wa Iran na kumpeleka Afrika ya Kati

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Mwanasheria wa mwanamke mmoja ambaye mwanaharakati wa demokrasia kutoka Iran amesema kuwa Marekani imemfukuza mteja wake na kumpeleka katika taifa la Central Africa Republic (CAR), na kusema ni hatua inayohatarisha maisha ya mteja wake.

    Kwa mujibu wa wakili huyo aliyezungumza na Reuters, Maisha mwanaharakati huyo yapo hatarini kutokana na vurugu na ukosefu wa amani ambao unashuhudia katika taifa hilo la Afrika ya Kati.

    Taasisi ya Iranian American Legal Defense Fund iliripoti kuwa wanawake watatu wa Iran waliokimbia nchi yao walikuwa katika hatari ya kufukuzwa kutoka Marekani.

    Pia unaweza kusoma:

  3. Abbas Araqchi: Makubaliano ya kumaliza vita na Marekani yako karibu kuafikiwa

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Iran, Abbas Araqchi, amesema kuwa makubaliano ya kumaliza vita kati ya Iran na Marekani yako katika hatua za mwisho, na kwamba Mlango bahari wa Hormuz utafunguliwa tena kama sehemu ya makubaliano hayo.

    Kwa mujibu wa BBC Persian, Araqchi alisema katika mahojiano ya televisheni kuwa “hatujawahi kuwa karibu hivi na makubaliano kama ilivyo sasa,” akiongezea kuwa makubaliano hayo yanaweza kuafikiwa ndani ya siku moja au mbili zijazo.

    Waziri huyo pia aliviambia vyombo vya habari nchini Iran kuepuka kutoa taarifa za uvumi ambazo zinaweza kuharibu mchakato huo wa kidiplomasia na kuathiri mazingira ya mazungumzo.

    Araqchi alisema kuwa makubaliano hayo yana ukurasa mmoja na nusu hadi mbili tu, lakini yamejadiliwa kwa zaidi ya miezi miwili, ambapo kila kipengele na kila sentensi imepitiwa na kuhaririwa kwa maslahi ya raia wa Iran.

    Pia unaweza kusoma:

  4. Jeshi la Marekani ladai kudungua ndege zisizo na rubani za Iran katika Mlango bahari wa Hormuz

    .

    Chanzo cha picha, US Navy via Getty Images

    Kituo kikuu cha kuendesha oparesheni za kijeshi Marekani (CENTCOM) imedai kuwa vikosi vyake vimeangusha ndege kadhaa zisizo na rubani zilizorushwa na Iran kuelekea Mlango bahari wa Hormuz.

    Katika taarifa iliyochapishwa kwenye mtandao wa X, CENTCOM ilisema Iran ilirusha ndege zisizo na rubani kadhaa kwa lengo la kulenga meli za kibiashara zilizokuwa zikisafiri kupitia Mlango bahari wa Hormuz.

    Taarifa hiyo iliongeza kuwa, "Vikosi vya Marekani vimedungua ndege hizo zote zisizo na rubani katika saa chache zilizopita, na usafiri wa meli kupitia Mlango wa Hormuz unaendelea bila usumbufu wowote."

    Centcom ilisema ndege hizo za Iran zilikuwa tishio kwa usalama wa meli za kibiashara zinazopitia eneo hilo.

    Pia unaweza kusoma:

  5. Hujambo na karibu katika matangazo yetu ya moja kwa moja Jumamosi ya leo