Moja kwa moja, Mlango wa Hormuz hautafunguliwa hadi Marekani ikubali masharti sita - Iran

Kauli hiyo inakuja wakati Iran na Oman zikisema mazungumzo kuhusu utaratibu mpya wa kuruhusu meli kupita katika Mlango wa Hormuz yamekuwa ya “chanya na yenye kujenga” katika siku za hivi karibuni.

Ruka Video uendelee
  • xx
  • Besigye
  • .
  • xx
  • xx
  • xx
  • Lungu
  • xx
  • xx
  • d
  • s
  • a
  • Sonko
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • Dangote
  • Lydia Wanjiku

Moja kwa moja

Na Mariam Mjahid

  1. FIFA yakosoa kampeni ya kutaka Infantino ajiuzulu

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    FIFA imekosoa vikali kile ilichokiita juhudi zinazoendelea za kuidhoofisha taasisi hiyo pamoja na rais wake, Gianni Infantino. Kauli hiyo imekuja baada ya ripoti zilizomuhusisha Infantino na madai kuhusu uhusiano wake wa kimapenzi, ambayo FIFA imesema ni madai yasiyo na msingi na ya uongo.

    Infantino pia anakabiliwa na shinikizo kutoka UEFA na baadhi ya vyama vya soka barani Ulaya kufuatia mpango wake uliositishwa wa FIFA Forward Enterprise, uliolenga kuanzisha kampuni mpya ya kusimamia haki za kibiashara na tiketi za FIFA, huku sehemu ya kampuni hiyo ikiuzwa kwa mwekezaji binafsi.

    Rais wa Shirikisho la Soka la Norway, Lise Klaveness, ametaka Infantino ajiuzulu, huku UEFA ikisema bado iko tayari kususia baadhi ya matukio ya FIFA ikiwa haitapewa uhakikisho kwamba mpango huo hautafufuliwa.

    FIFA imemtetea Infantino ikisema alichaguliwa kidemokrasia na vyama wanachama na anaendelea kuhudumu kwa mamlaka waliompa. Shirikisho hilo limeonya kwamba wanaopinga uongozi wake wanapaswa kutumia taratibu rasmi za kidemokrasia za FIFA badala ya madai au taarifa potofu.

    Upinzani dhidi ya Infantino unatoka zaidi Ulaya, huku Mexico, Conmebol na CAF zikimuunga mkono. CAF, inayowakilisha nchi 54 za Afrika, imesema inaunga mkono Infantino kwa kauli moja.

  2. Masharti ya Iran yapunguza matumaini ya kufikiwa haraka kwa makubaliano

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Masharti yaliyotolewa na Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran, Mohammad Baqer Zolghadr, kwa kiasi kikubwa yanarudia masharti yaliyokuwa sehemu ya makubaliano ya mfumo yaliyofikiwa kati ya Iran na Marekani mwezi Juni. Lakini sasa, Zolghadr ameyawasilisha masharti hayo kama sharti la lazima ili Mlango wa Hormuz urejee kufanya kazi kikamilifu kama kawaida.

    Masharti hayo yanajumuisha kuondolewa kwa baadhi ya vikwazo dhidi ya Iran, kulipwa fidia kwa uharibifu uliosababishwa na vita, pamoja na kusitishwa mara moja kwa kizuizi cha Marekani dhidi ya bandari za Iran.

    Iwapo kauli hizo zitatumika kama ishara ya msimamo wa sasa wa Tehran, huenda zikapunguza zaidi matumaini ambayo Rais wa Marekani Donald Trump alikuwa ameyaibua kuhusu uwezekano wa kufikiwa kwa makubaliano na Iran hivi karibuni.

    Wakati huo huo, Iran na Oman zinaendelea na mazungumzo kuhusu njia mpya ya kuruhusu meli kupita katika Mlango wa Hormuz. Mpango huo unatarajiwa kusimamiwa kwa pamoja na Iran na Oman, huku nchi hizo zikitoza ada kwa matumizi ya njia hiyo.

    Makubaliano kama hayo, iwapo yatafikiwa, yangefungua sehemu tu ya njia kuelekea suluhisho pana la mzozo huo. Hata hivyo, yanaweza kumpa Donald Trump njia ya kujiondoa katika vita bila kuhitaji kufikia mara moja makubaliano kamili ya kumaliza mzozo.

    tofauti hizo ni za aina gani.

  3. Mlango wa Hormuz hautafunguliwa hadi Marekani ikubali masharti sita - Iran

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran, Mohammad Bagher Zolghadr, amesema Iran haitafungua tena Mlango wa Hormuz hadi Marekani itakapokubali masharti sita yaliyowekwa na Tehran.

    Masharti hayo yanajumuisha kupunguza vikwazo dhidi ya Iran, kulipa fidia za uharibifu wa vita, kusitisha mara moja kizuizi cha majini dhidi ya bandari za Iran, kuacha vitisho dhidi ya Iran na kuachilia mali za Iran zilizogandishwa. Kauli yake inaashiria msimamo mkali zaidi wa Tehran katika mazungumzo kuhusu ufunguzi wa njia hiyo muhimu ya mafuta.

    Kauli hiyo inakuja wakati Iran na Oman zikisema mazungumzo kuhusu utaratibu mpya wa kuruhusu meli kupita katika Mlango wa Hormuz yamekuwa ya “chanya na yenye kujenga” katika siku za hivi karibuni. Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi, amesema mazungumzo hayo yako katika hatua za mwisho, lakini amesisitiza kuwa makubaliano hayatamaanisha mlango huo utafunguliwa mara moja, kwa kuwa ufunguzi wake utategemea masharti mengine.

    Ripoti ya Axios siku moja kabla ilisema, ikinukuu mwanadiplomasia kutoka moja ya nchi zinazosaidia upatanishi, kwamba wajumbe wa Iran walikuwa wakisubiri idhini ya mwisho kutoka Baraza Kuu la Usalama wa Taifa ili kukamilisha makubaliano na Oman pamoja na Marekani. Mwanadiplomasia huyo alisema idhini hiyo ilitarajiwa kutolewa “hivi karibuni”.

    Reuters pia iliripoti, ikimnukuu afisa wa Marekani, kwamba kumekuwa na maendeleo katika mazungumzo kati ya Iran na Oman na Washington inatarajia makubaliano kufikiwa hivi karibuni.

    Kwa mujibu wa afisa huyo wa Marekani, Washington itaondoa kizuizi dhidi ya bandari za Iran baada ya kutangazwa kwa makubaliano yatakayohakikisha meli za kibiashara zinapita bila kizuizi katika Mlango wa Hormuz. Kauli ya Zolghadr ni muhimu kwa sababu ametoka katika taasisi hiyo hiyo inayotarajiwa kutoa uamuzi wa mwisho kwa upande wa Iran kuhusu makubaliano hayo.

    Wakati huo huo, kuna taarifa kwamba Zolghadr amewasilisha barua ya kujiuzulu kutoka nafasi yake, lakini Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, amepinga hatua hiyo na kumuomba aendelee na kazi. Pezeshkian alipoulizwa kuhusu taarifa hizo amesema kuna “tofauti kadhaa” ambazo wanaendelea kujaribu kuzitatua, bila kueleza zaidi tofauti hizo ni za aina gani.

  4. Salaam na karibu katika habari zetu za moja kwa moja leo 09.08.2026