Vieira ajiunga Hamburg kwa uhamisho wa kudumu

Chanzo cha picha, Getty Images
Kiungo wa Arsenal, Fabio Vieira, amejiunga na klabu ya Bundesliga ya Hamburg kwa uhamisho wa kudumu.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alikuwa Hamburg kwa mkopo msimu wa 2025-26, baada ya awali pia kucheza kwa mkopo katika klabu yake ya zamani, Porto.
Vieira alicheza mechi 49 akiwa na Arsenal katika mashindano yote na kufunga mabao saba pamoja na kutoa pasi tano za mabao.
Akiwa Hamburg, alisaidia klabu hiyo kurejea Bundesliga baada ya miaka saba na sasa ameondoka Arsenal moja kwa moja kujiunga na klabu hiyo.
Miongoni mwa kumbukumbu zake kubwa akiwa Arsenal ni kufunga penati ya ushindi katika mikwaju ya penali dhidi ya Manchester City, iliyoiwezesha Arsenal kutwaa Ngao ya Jamii ya 2023 katika Uwanja wa Wembley.



