Kombe la Dunia: DRC yalazwa na Colombia

Chanzo cha picha, Reuters
Katika mechi ya mwisho siku ya Jumanne, timu ya soka ya Colombia ilifanikiwa kuishinda DRC Congo kwa bao moja na kujihakikishia kusonga mbele kwa pointi 6.
Colombia walianza mchezo kwa kasi kuanzia dakika za kwanza kabisa, na mshambuliaji wa timu hiyo Luis Diaz, alifunga dakika ya 10, lakini mwamuzi akatangaza kuwa ameotea.
Diaz pia alifunga bao zuri mwishoni mwa kipindi cha pili baada ya kuwapiga chenga walinzi kadhaa wa Congo, lakini mwamuzi akakataa tena kuwa ameotea mara tu alipopata pasi.
Mchezaji wa Colombia Mones, hatahivyo aliifungia Colombia bao la pekee katika dakika ya 76.
Hivyo, Colombia, ambayo ilikuwa imeishinda Uzbekistan katika mechi ya kwanza, ilipata pointi 6 kupitia ushindi huo na kuwaweka kileleni mwa jedwali juu ya Ureno na kusonga mbele.
Soma:

















