Netanyahu asema makubaliano ya Israel na Lebanon ni pigo kwa Iran na Hezbollah

Chanzo cha picha, Reuters
Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa Israel, ameyakaribisha makubaliano yaliyofikiwa kati ya Israel na Lebanon kwa upatanishi wa Marekani, akiyataja kuwa "ushindi wa kihistoria" na kusema ni "pigo kwa Iran na Hezbollah."
"Jana, baada ya mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Israel na Lebanon, tulifikia makubaliano ya kihistoria yanayoinufaisha serikali ya Israel. Makubaliano haya ni pigo kwa Iran na Hezbollah," Netanyahu alisema katika hotuba iliyorushwa na televisheni.
Netanyahu pia alisisitiza kuwa majeshi ya Israel yataendelea kuwepo katika eneo aliloliita "ukanda wa usalama," ambalo ni eneo lililoanzishwa na vikosi vya Israel ndani ya Lebanon, takribani kilomita 10 kutoka mpakani.
Waziri Mkuu huyo alisema: "Tutabaki katika eneo hili hadi Hezbollah na makundi mengine tunayoyachukulia kuwa ya kigaidi yatakapovuliwa silaha."
Aliongeza kuwa Marekani na Lebanon zinatambua haki ya Israel kuendelea kuwa na ukanda wa usalama ndani ya ardhi ya Lebanon kwa muda utakaohitajika ili kuhakikisha usalama wake.
Soma Zaidi:





