Moja kwa moja, Trump aonya Iran itaangamizwa kabisa ikiendelea kukiuka makubaliano ya kusitisha mapigano

Baada ya mashambulizi hayo ya pande zote mbili, Marekani na Iran zilishutumiana kwa kukiuka makubaliano ya kusitisha mapigano.

Moja kwa moja

Na Mariam Mjahid

  1. Netanyahu asema makubaliano ya Israel na Lebanon ni pigo kwa Iran na Hezbollah

    f

    Chanzo cha picha, Reuters

    Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa Israel, ameyakaribisha makubaliano yaliyofikiwa kati ya Israel na Lebanon kwa upatanishi wa Marekani, akiyataja kuwa "ushindi wa kihistoria" na kusema ni "pigo kwa Iran na Hezbollah."

    "Jana, baada ya mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Israel na Lebanon, tulifikia makubaliano ya kihistoria yanayoinufaisha serikali ya Israel. Makubaliano haya ni pigo kwa Iran na Hezbollah," Netanyahu alisema katika hotuba iliyorushwa na televisheni.

    Netanyahu pia alisisitiza kuwa majeshi ya Israel yataendelea kuwepo katika eneo aliloliita "ukanda wa usalama," ambalo ni eneo lililoanzishwa na vikosi vya Israel ndani ya Lebanon, takribani kilomita 10 kutoka mpakani.

    Waziri Mkuu huyo alisema: "Tutabaki katika eneo hili hadi Hezbollah na makundi mengine tunayoyachukulia kuwa ya kigaidi yatakapovuliwa silaha."

    Aliongeza kuwa Marekani na Lebanon zinatambua haki ya Israel kuendelea kuwa na ukanda wa usalama ndani ya ardhi ya Lebanon kwa muda utakaohitajika ili kuhakikisha usalama wake.

    Soma Zaidi:

  2. Ethiopia mwenyeji mkutano wa kimkakati kujadili mwelekeo mpya wa diplomasia ya umma Afrika

    h

    Chanzo cha picha, WPA

    Watu zaidi ya 600, wakiwemo viongozi wa kimataifa, wanadiplomasia, watunga sera, wabunifu, wafanyabiashara, wasomi na wawakilishi wa mashirika ya kiraia kutoka Afrika na sehemu nyingine za dunia, wanatarajiwa kukutana jijini Addis Ababa, Ethiopia, tarehe 29 na 30 Julai kwa ajili ya mkutano wa World Public Summit Africa.

    Mkutano huo wa kimataifa unalenga kuimarisha diplomasia ya umma na kuongeza mchango wa Afrika katika kuunda mustakabali wa dunia.

    Rais wa Ethiopia, Taye Atske Selassie anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika mkutano huo wenye kauli mbiu “ Dunia mpya: Afrika itavyobadili mwelekeo wa siku zijazo” ambao unakuja wakati ambapo mataifa ya Afrika yanazidi kutafuta nafasi kubwa zaidi katika maamuzi ya kimataifa.

    Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Jukwaa la World Peoples Assembly, mfumo wa awali wa kidiplomasia unaozingatia serikali kwa serikali pekee haukidhi tena mahitaji ya dunia ya sasa badala yake, wanasisitiza umuhimu wa kuwashirikisha wananchi, asasi za kiraia, taasisi za elimu, sekta binafsi na wadau wa utamaduni katika kujenga mahusiano ya kimataifa.

    "Mkutano huu unaakisi mtazamo mpya wa ushirikiano wa kimataifa unaoweka mbele ushirikiano kati ya watu, kuheshimiana na malengo ya pamoja ya maendeleo," inaeleza taarifa ya waandalizi.

  3. Timu ya taifa ya Iran yaaga Kombe la Dunia

    f

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Mchezo wa hatua ya makundi wa Kombe la Dunia kati ya Algeria na Austria ulimalizika kwa sare ya mabao 3 kwa 3, matokeo yaliyofuta kabisa matumaini ya mwisho ya timu ya taifa ya Iran kufuzu hatua ya mtoano.

    Marko Arnautović aliifungia Austria bao la kwanza katika dakika ya 28, kabla ya Algeria kusawazisha kupitia Belkhali katika dakika ya 45.

    Marcel Sabitzer aliirejeshea Austria uongozi katika dakika ya 55, lakini Riyad Mahrez akaifungia Algeria bao la pili la kusawazisha.

    Algeria ilipata bao la tatu katika dakika ya 90+3, lakini Austria ilisawazisha tena katika dakika ya 90+5.

    Kutokana na matokeo hayo, Iran ilishindwa kujipanga miongoni mwa timu zilizofuzu kama washindi wa makundi au miongoni mwa timu bora za nafasi ya tatu, na hivyo kuaga rasmi Kombe la Dunia.

    Maelezo zaidi:

  4. Idadi ya waliofariki dunia katika matetemeko ya ardhi Venezuela yafikia 1,400

    f

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Siku tatu baada ya matetemeko mawili makubwa ya ardhi kuikumba Venezuela, juhudi kubwa za uokoaji bado zinaendelea. Idadi ya vifo vilivyothibitishwa imevuka watu 1,400, huku watu wengi wakiendelea kutoweka.

    Wakati huo huo, hali ya kutoridhishwa na mwitikio wa serikali inaongezeka miongoni mwa wananchi.

    Mwandishi wa BBC aliyepo mjini La Guaira, eneo lililoathirika zaidi, anasema hali ni mbaya, huku idadi isiyojulikana ya wakazi ikihofiwa kuwa bado imekwama chini ya vifusi vya majengo yaliyoporomoka.

    Makundi ya kimataifa ya kutoa misaada pia yamewasili katika eneo hilo, na timu za uokoaji kutoka Mexico, Brazil na mataifa mengine zinaendelea kufanya kazi usiku na mchana kusaidia shughuli za uokoaji na utoaji wa misaada.

    Maelezo zaidi:

  5. DRC watinga hatua ya mtoano kwa mara ya kwanza katika Kombe la Dunia

    g

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Timu ya taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, maarufu kama Leopards, imefuzu kwa mara ya kwanza katika hatua ya mtoano ya Kombe la Dunia baada ya kuichapa Uzbekistan mabao 3 kwa 1 mjini Houston.

    Yoane Wissa alifunga mabao mawili, huku Fiston Mayele akiongeza bao moja, na kuiongoza DR Congo kubadili matokeo baada ya kujikuta nyuma mapema.

    Ushindi huo ulizua shamrashamra kubwa katika Kinshasa, ambapo mashabiki walisherehekea hatua hiyo ya kihistoria ya timu yao kufuzu kwa mara ya kwanza zaidi ya hatua ya makundi.

    Kwa taifa ambalo lilikuwa halijashiriki Kombe la Dunia tangu mwaka 1974, mafanikio hayo yana uzito mkubwa, yakirejesha fahari na matumaini katika nchi ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikikabiliwa na changamoto za kiusalama.

    Matokeo hayo yameandika historia, yakikomesha kusubiri kwa miaka 52 tangu DR Congo iliposhiriki kwa mara ya mwisho Kombe la Dunia, na sasa Chui watakutana na timu ya England katika hatua ya 32 bora jijini Atlanta Jumatano ijayo.

    Soma pia:

  6. Trump aonya Iran itaangamizwa kabisa ikiendelea kukiuka makubaliano ya kusitisha mapigano

    f

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kwamba ndege za kivita za Marekani zimeshambulia maghala ya makombora na ndege zisizo na rubani za Iran pamoja na vituo vya rada katika maeneo ya pwani.

    Trump amesema mashambulizi hayo yalifanyika kujibu kile alichokitaja kuwa "ukiukaji wa mara kwa mara wa makubaliano ya kusitisha mapigano" na akaonya kwamba ikiwa Marekani italazimika "kukamilisha" operesheni zake za kijeshi, basi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitakuwepo tena.

    Kwa upande mwingine, Islamic Revolutionary Guard Corps (IRGC) imetangaza kwamba imelenga vituo vya kijeshi vya Marekani katika kambi ya Ali al Salem nchini Kuwait na makao makuu ya Kikosi cha Tano cha Jeshi la Wanamaji la Marekani nchini Bahrain kwa kutumia makombora ya masafa marefu na ndege zisizo na rubani.

    IRGC pia imeonya kwamba itachukua hatua kali zaidi dhidi ya meli inazozitaja kuwa "zinazokiuka" masharti yaliyowekwa.

    Baada ya mashambulizi hayo ya pande zote mbili, Marekani na Iran zilishutumiana kwa kukiuka makubaliano ya kusitisha mapigano.

    Katika taarifa yake, Centcom ilisema: "Iran ilipewa fursa ya kuheshimu makubaliano ya kusitisha mapigano, lakini ilichagua kutofanya hivyo wakati vikosi vyake viliporusha ndege isiyo na rubani ya kujitoa mhanga iliyogonga meli ya mafuta ya MT Kiku," meli iliyosajiliwa nchini Panama.

    Maelezo zaidi:

  7. Hujambo na karibu kwa matangazo ya moja kwa moja ya taarifa zinazochipuka kote duniani.