Iran yamteua kiongozi mpya wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa
Iran imemteua kiongozi mpya wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa, katika mabadiliko muhimu ya uongozi wakati nchi hiyo ikikabiliana na mzozo kati yake, Marekani na Israel.
Mohsen Rezaei, kamanda wa zamani wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, ameteuliwa kushika wadhifa huo wenye jukumu muhimu katika kuamua namna Iran itakavyokabiliana na mzozo huo.
Rezaei amewahi kusema Iran inapaswa kudumisha udhibiti wa Mlango wa Hormuz, akisema hilo ni muhimu zaidi kuliko kumiliki silaha za nyuklia.
Kwa kuzingatia historia yake ndefu ya kushika nyadhifa za juu serikalini, uteuzi wake unaonekana kuashiria kuwa kizazi cha zamani cha wanasiasa wa Iran bado kinaendelea kuwa na ushawishi mkubwa katika uongozi wa nchi hiyo.
Hata hivyo, kumekuwa na utabiri kwamba wanasiasa vijana wanaweza kuanza kupewa nyadhifa za juu katika uongozi wa Iran.
Soma Zaidi Hapa: