Kombe la Dunia 2026: Afrika Kusini yalalamikia kucheleweshwa kwa viza ya wachezaji wake

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images
Waziri wa michezo wa Afrika Kusini amekerwa na tukio la kucheleweshwa kwa hati ya usafiri ya timu ya soka ya nchi hiyo kuelekea Mexico kabla ya michuano ya Kombe la Dunia .
Shirika la utangazaji la taifa SABC lilisema hali hiyo imewafanya baadhi ya wachezaji kunyimwa viza. Hakuna maelezo mengine yaliyotolewa.
Akijibu, waziri wa michezo Gayton McKenzie alisema aliambia Shirikisho la Soka la Afrika Kusini (Safa) "Nimeomba kupewa maelezo na lazima hatua zichukuliwe dhidi ya waliohusika na sintofahamu hii".
"Tunafanywa kuonekana kama wapumbavu," aliongeza kwenye X. Safa bado haijatoa tamko lolote kuhusiana na suala hilo.
Timu hiyo maarufu Bafana Bafana, inatarajiwaa kumenyana na Jamaica katika mechi ya kirafiki nchini Mexico siku ya Ijumaa.
Kisha watacheza mechi ya ufunguzi wa Kombe la Dunia dhidi ya Mexico, ambayo ni mwenyeji wa mashindano hayo pamoja na Marekani na Canada, tarehe 11 Juni.
Afrika Kusini ni mojawapo ya mataifa 10 ya Afrika yanayoshiriki katika Kombe la Dunia litakalojumuisha timu 48.
Pia unaweza kusoma:




