UAE yazima mashambulizi ya makombora na droni za Iran
Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) imesema mifumo yake ya ulinzi wa anga ilikuwa ikikabiliana na mashambulizi ya makombora na droni kutoka Iran mapema leo Ijumaa, katika mzozo unaoendelea mashambulizi yanayotikisa usitishaji wa vita uliotangazwa kati ya Marekani na Iran.
Tukio hilo limekuja wakati mvutano katika eneo la Mlango wa Hormuz ukiendelea kuongezeka, kufuatia mapigano ya mara kwa mara kati ya pande hizo mbili na washirika wao katika Ghuba ya Uajemi.
Marekani imesema hakuna uharibifu uliotokea kwa meli zake za kijeshi baada ya mashambulizi ya hivi karibuni, huku Rais Donald Trump akisisitiza kuwa sitisho la vita bado linaendelea licha ya mivutano hiyo.
Iran kwa upande wake imeilaumu Marekani kwa kuvunja makubaliano ya kusitisha mapigano na kusema ilijibu mashambulizi dhidi ya maeneo yake na meli zake katika eneo la Hormuz.
Baada ya saa kadhaa za mapigano, ripoti kutoka UAE na Iran zilisema hali katika maeneo yaliyoathirika imerejea kuwa ya kawaida, huku pande zote zikiendelea kuilaumiana kuhusu nani alikiuka makubaliano ya kusitisha vita.