Uingereza na washirika waweka vikwazo dhidi ya “mitandao” inayosaidia vurugu za walowezi Ukingo wa Magharibi

Chanzo cha picha, Reuters
Uingereza, Australia, Canada, Ufaransa na Norway zimeweka vikwazo dhidi ya kile wanachokiita “mitandao” inayohusika na kufadhili na kuwezesha mashambulizi dhidi ya raia wa Palestina na walowezi wa Kiyahudi katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa na Israel.
Hatua hiyo inalenga “kuwawajibisha walowezi wenye misimamo mikali kwa viwango vya kutisha vya vurugu za walowezi,” nchi hizo tano zimesema.
Ufaransa pia imepiga marufuku kuingia nchini humo kwa Waziri wa Fedha wa Israel mwenye misimamo mikali, Bezalel Smotrich, ambaye ana mamlaka makubwa kuhusu sera za serikali za makazi ya walowezi katika Ukingo wa Magharibi, ambayo ni haramu chini ya sheria ya kimataifa.
Israel imesema inakataa “hatua hizo za aibu,” zikiziita kuwa ni za kisiasa.
Israel imejenga takribani makazi 160 yanayowahifadhi Wayahudi wapatao 700,000 tangu ilipouteka Ukingo wa Magharibi na Jerusalem Mashariki, ardhi inayotakiwa na Wapalestina kwa ajili ya taifa lao la baadaye pamoja na Gaza, wakati wa vita vya Mashariki ya Kati mwaka 1967. Inakadiriwa Wapalestina milioni 3.3 wanaishi pamoja nao.
Kumekuwa na ongezeko la mashambulizi ya walowezi dhidi ya Wapalestina na mali zao katika Ukingo wa Magharibi tangu kuanza kwa vita vya Gaza, vilivyochochewa na shambulio la Hamas dhidi ya Israel tarehe 7 Oktoba 2023.
UN imeandika mashambulizi 1,835 ya walowezi dhidi ya Wapalestina mwaka 2025 yaliyosababisha majeruhi au uharibifu wa mali katika takribani jamii 280 za Ukingo wa Magharibi.
Takribani Wapalestina saba waliuawa na 832 kujeruhiwa katika mashambulizi hayo, idadi zote mbili zikiongezeka kwa asilimia 130 ikilinganishwa na mwaka uliopita.
Unaweza kusoma;














