Korea Kaskazini yasema mpango wake wa nyuklia hauko kwenye mazungumzo

Chanzo cha picha, Getty Images
Kim Yo-jong, dada wa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un, amesema katika taarifa kwamba mpango wa nyuklia wa nchi hiyo “hauwezi kujadiliwa kabisa”.
“Taasisi yetu kuhusu nguvu za nyuklia haiwezi kujadiliwa kwa namna yoyote,” alisema katika taarifa hiyo iliyochapishwa na gazeti rasmi la chama tawala, Rodong Sinmun.
Aliongeza pia kuwa Korea Kaskazini “haitavumilia vitisho vyovyote”.
Kim Yo-jong, ambaye ni mmoja wa viongozi muhimu katika masuala ya mawasiliano na sera za nje za Korea Kaskazini, ameoa kauli hizo kabla ya ziara ya Rais wa China Xi Jinping nchini Korea Kaskazini, inayotarajiwa kuanza Jumatatu na kuendelea hadi Jumanne, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya serikali.
Ziara hiyo ya Xi Jinping mjini Pyongyang itakuwa ya kwanza katika kipindi cha miaka saba.
Hii inakuja baada ya rais huyo wa China kufanya mfululizo wa mikutano na Rais wa Marekani Donald Trump na Rais wa Urusi Vladimir Putin mwezi uliopita.
China inachukuliwa kuwa mmoja wa washirika muhimu zaidi wa kisiasa na kiuchumi wa Korea Kaskazini.
Soma zaidi:







