Moja kwa moja, Urusi yashambulia treni ya Ukraine muda mfupi baada ya Boris Johnson na maafisa wakuu wa Ulaya kuondoka kituoni
Droni ya Urusi imegonga treni karibu na mpaka wa Ukraine na Poland muda mfupi baada ya aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza, Boris Johnson, na maafisa wakuu wa usalama wa Ulaya kupita eneo hilo.
Muhtasari
Bayern Munich wamnyatia Florian Wirtz wa Liverpool
Urusi yashambulia treni ya Ukraine muda mfupi baada ya Boris Johnson na maafisa wakuu wa Ulaya kuondoka kituoni
Moja kwa moja
Abdalla Seif Dzungu
Saudi Arabia yaonya raia wake katika maeneo mawili yanayopakana na Yemen
Chanzo cha picha, EPA
Maelezo ya picha, Wahouthi
Shirika la
Ulinzi wa Raia la Saudi Arabia lilitoa maonyo siku ya Jumapili kuhusu
mashambulizi yanayowezekana katika maeneo mawili yanayopakana na Yemen.
Maonyo haya,
yaliyotolewa kwa ajili ya mji wa Abha na eneo linalozunguka mji wa Khamis
Mushait, yalifutwa haraka.
Maonyo hayo
yalitolewa muda mfupi baada ya vyombo vya habari vya Houthi kuripoti
mashambulizi ya Saudi Arabia kaskazini mwa Yemen, karibu na mpaka.
Mgogoro kati
ya Houthi wanaoungwa mkono na Iran na vikosi vya serikali ya Yemen vinavyoungwa
mkono na Saudi Arabia umeongezeka tangu wiki iliyopita.
Baada ya
Houthi kutangaza kizuizi cha majini mnamo Julai 20 kujibu kizuizi
cha Saudi Arabia, mgogoro wao na vikosi vya serikali ya Yemen umeongezeka.
Wiki
iliyopita, Houthi walichukua udhibiti kamili wa pwani ya magharibi ya Bahari
Nyekundu na Mlango-Bab al-Mandab katika shambulio kubwa, na kuwafukuza
wanajeshi wa serikali.
Bayern Munich wamnyatia Florian Wirtz wa Liverpool
Chanzo cha picha, Getty Images
Bayern Munich wanafuatilia kwa karibu kiungo wa Ujerumani Florian
Wirtz, mwenye umri wa miaka 23, katika klabu ya Liverpool. (Teamtalk)
Liverpool inaweza kuvunja rekodi yake ya usajili kwa kumsajili
mshambuliaji wa Brazil wa Bournemouth, Rayan, mwenye umri wa miaka 20, msimu
ujao. Timu hiyo italazimika kulipa pauni milioni 130 iwapo itaamua kutumia
kipengele cha mkataba kinachomruhusu mchezaji huyo kuondoka kwa kiasi hicho.
Kifungu hicho kitaanza kutumika mwaka 2027. (Football Insider)
Liverpool wana kipengele cha kulipa euro milioni 55 (£47.2m)
ili kumsajili moja kwa moja beki wa Uruguay Ronald Araujo, mwenye umri wa miaka
27, baada ya kumchukua kwa mkopo kutoka Barcelona. (Fabrizio Romano via Caught
Offside)
Juventus haiko tayari kumuuza Pierre Kalulu katika dirisha
la usajili la Januari, licha ya Manchester United na Liverpool kuhusishwa na
uwezekano wa kumsajili beki huyo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 26. (Manchester
Evening News)
Kocha wa Borussia Dortmund, Niko Kovac, ameondoa uwezekano
wa klabu hiyo kumsajili tena winga wa zamani wa Manchester United, Jadon
Sancho, mwenye umri wa miaka 26, ambaye kwa sasa hana klabu. (Mirror)
Wakala wa Sancho amefanya mazungumzo na klabu kadhaa za Ligi
Kuu England kuhusu uwezekano wa mchezaji huyo kujiunga na moja ya klabu hizo. (Football
Insider),
Borussia Dortmund imeungana na Manchester United kuonyesha
nia ya kumsajili kiungo wa Leicester City, Louis Page, huku klabu hiyo ya
Ujerumani ikiwa imetuma maskauti kumfuatilia Mwingereza huyo mwenye umri wa
miaka 18. (Teamtalk),
Klabu za Championship pamoja na Celtic zinafikiria kumsajili
beki wa Liverpool na timu ya taifa ya vijana ya England, Luke Chambers, mwenye
umri wa miaka 22, katika dirisha la usajili la Januari. (Football Insider)
Aliyekuwa mkurugenzi wa michezo wa Inter Milan, Piero
Ausilio, anatarajiwa kujiunga na Tottenham, ambayo imempa Muitaliano huyo
mwenye umri wa miaka 54 nafasi ya kazi kuanzia dirisha la usajili la Januari. (Gazzetta)
Urusi yashambulia treni ya Ukraine muda mfupi baada ya Boris Johnson na maafisa wakuu wa Ulaya kuondoka kituoni
Droni ya
Urusi imegonga treni karibu na mpaka wa Ukraine na Poland muda mfupi baada ya
aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza, Boris Johnson, na maafisa wakuu wa usalama
wa Ulaya kupita hapo.
Hakuna
majeruhi walioripotiwa kufuatia shambulio hilo huko Yahodyn, ambalo lililenga
injini ya treni hiyo. Abiria wote walikuwa wameshaondolewa, kulingana na
maafisa wa Ukraine.
Johnson na
washauri wengine wa usalama wa kitaifa wa Ulaya, akiwemo Jonathan Powell wa
Uingereza, walikuwa wamepita kwenye njia hiyo hiyo kwa treni tofauti walipokuwa
wakirejea kutoka kwenye mkutano mjini Kyiv.
Urusi
ilisema ilishambulia "miundombinu ya reli" magharibi mwa Ukraine,
lakini kampuni ya reli ya serikali ya Ukraine, Ukrzaliznytsia, ilisema kuwa
"kuna uwezekano mkubwa kuwa lengo la droni hiyo lilikuwa treni ya
kidiplomasia".
Katika
taarifa, ilisema treni hiyo "ilikuwa imeondoka kituoni mapema kuliko
ilivyotarajiwa kutokana na mabadiliko ya ratiba... kufuatia vitisho vya mara
kwa mara vya mashambulizi ya Urusi".
Pia ilisema
agizo la kuwaondoa abiria kwenye treni iliyoshambuliwa lilitolewa "dakika
15 tu" kabla ya shambulio hilo lililofanywa na droni ya Urusi inayotumia
injini ya ndege.
Mamlaka ya
reli pia ilisema kuwa aliyekuwa mkuu wa CIA, David Petraeus, alikuwa ndani ya
treni nyingine katika kituo cha Yahodyn wakati wa shambulio hilo la droni.
Maafisa wa
Ukraine na Poland walisema droni hiyo ya Urusi ilishambulia eneo lililoko
umbali wa kilomita 2 kutoka mpaka wa Poland.
Chanzo cha picha, Getty Images
Natumai hujambo na karibu katika habari zetu za moja kwa moja