Moja kwa moja, Marekani yasema inaweza kuendelea na zuio la majini dhidi ya Iran bila ukomo

Kauli hiyo inakuja wakati mazungumzo ya kusitisha vita yakikwama, huku usafirishaji wa mafuta duniani ukiathiriwa na mzozo unaoendelea katika eneo la Mlango wa Hormuz.

Muhtasari

Marekani yasema inaweza kuendelea na zuio la majini dhidi ya Iran bila ukomo

Ruka Video uendelee
  • xx
  • Besigye
  • .
  • xx
  • xx
  • xx
  • Lungu
  • xx
  • xx
  • d
  • s
  • a
  • Sonko
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • Dangote
  • Lydia Wanjiku

Moja kwa moja

Na Mariam Mjahid

  1. Trump atangaza ushuru wa hadi asilimia 100 kwa ndege zisizo na rubani zinazoagizwa kutoka nje

    D

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza ushuru wa hadi asilimia 100 kwa ndege zisizo na rubani zinazoagizwa kutoka nje pamoja na baadhi ya vipuri vyake.

    Kwa mujibu wa tangazo hilo, ndege kubwa zisizo na rubani zenye uzito wa zaidi ya kilo 25 na zilizo na teknolojia zinazohusishwa na usalama wa taifa, ikiwemo kamera za joto na vituo vya kuziendeshea, zitatozwa ushuru wa asilimia 100.

    Ndege ndogo zisizo na rubani zitatozwa ushuru wa asilimia 25, huku ushuru huo ukitarajiwa kuanza kutekelezwa Septemba 3.

    Utawala wa Trump unasema hatua hiyo inalenga kuhamasisha uzalishaji wa ndege hizo na vipuri vyake nchini Marekani, pamoja na kupunguza utegemezi wa minyororo ya ugavi ya nje, hususan China.

    Mamlaka za Marekani zimeeleza kuwa ndege zisizo na rubani zina matumizi ya kibiashara, lakini pia zinaweza kutumika katika shughuli za kijeshi na kiusalama, ikiwemo ufuatiliaji, ukusanyaji wa taarifa nyeti na mashambulizi.

    Hatua hiyo huenda ikaongeza gharama kwa waagizaji, watumiaji na kampuni zinazotegemea ndege hizo pamoja na vipuri vinavyotengenezwa nje ya Marekani.

    Soma Zaidi;

  2. Marekani yasema inaweza kuendelea na zuio la majini dhidi ya Iran bila ukomo

    D

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Marekani imesema inaweza kuendelea na mzingiro wake wa kijeshi dhidi ya Iran kwa muda usiojulikana, huku ikiendelea kuongeza shinikizo la kiuchumi kwa Tehran.

    Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Pete Hegseth, amesema jeshi la Marekani lina uwezo wa kuendeleza mzingiro huo kwa muda wowote unaohitajika kwa kubadilisha meli za kivita zinazopelekwa katika eneo hilo.

    Kauli hiyo inakuja wakati mazungumzo ya kusitisha vita yakikwama, huku usafirishaji wa mafuta duniani ukiathiriwa na mzozo unaoendelea katika eneo la Mlango wa Hormuz.

    Makamu wa Rais wa Marekani, JD Vance, amesema malengo makuu ya Washington katika mzozo huo ni kuhakikisha bei za nishati zinabaki katika viwango vinavyoweza kumudu Wamarekani, kuzuia Iran kupata silaha za nyuklia na kuhakikisha Marekani inakuwa katika nafasi imara zaidi kimkakati.

    Rais Donald Trump amekuwa akisisitiza kuwa Marekani inadhibiti kikamilifu Mlango wa Hormuz, wakati Iran ikisema njia hiyo itaendelea kufungwa hadi masharti yake yatimizwe.

    Waziri wa Hazina wa Marekani, Scott Bessent, amesema Washington iko tayari kuchukua hatua za kiuchumi dhidi ya Iran ambazo hazijawahi kutekelezwa katika historia ya kuitenga nchi kiuchumi.

    Bessent amesema Marekani itatangaza hatua zaidi wiki ijayo, huku ikilenga kuongeza shinikizo la kiuchumi kwa Tehran.

    Soma Zaidi Hapa:

  3. Hujambo na karibu kwa matangazo ya moja kwa moja ya tarehe 14/08/2026.