Trump atangaza ushuru wa hadi asilimia 100 kwa ndege zisizo na rubani zinazoagizwa kutoka nje

Chanzo cha picha, Getty Images
Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza ushuru wa hadi asilimia 100 kwa ndege zisizo na rubani zinazoagizwa kutoka nje pamoja na baadhi ya vipuri vyake.
Kwa mujibu wa tangazo hilo, ndege kubwa zisizo na rubani zenye uzito wa zaidi ya kilo 25 na zilizo na teknolojia zinazohusishwa na usalama wa taifa, ikiwemo kamera za joto na vituo vya kuziendeshea, zitatozwa ushuru wa asilimia 100.
Ndege ndogo zisizo na rubani zitatozwa ushuru wa asilimia 25, huku ushuru huo ukitarajiwa kuanza kutekelezwa Septemba 3.
Utawala wa Trump unasema hatua hiyo inalenga kuhamasisha uzalishaji wa ndege hizo na vipuri vyake nchini Marekani, pamoja na kupunguza utegemezi wa minyororo ya ugavi ya nje, hususan China.
Mamlaka za Marekani zimeeleza kuwa ndege zisizo na rubani zina matumizi ya kibiashara, lakini pia zinaweza kutumika katika shughuli za kijeshi na kiusalama, ikiwemo ufuatiliaji, ukusanyaji wa taarifa nyeti na mashambulizi.
Hatua hiyo huenda ikaongeza gharama kwa waagizaji, watumiaji na kampuni zinazotegemea ndege hizo pamoja na vipuri vinavyotengenezwa nje ya Marekani.
Soma Zaidi;





















