Trump alisuta bunge la Marekani kwa kusitisha hatua za kijeshi dhidi ya Iran: Hii ni kumsaidia adui
Rasi wa Marekani Donald Trump amekosoa vikali kura ya Seneti ya Marekani kuhusu azimio la kutaka kusitishwa kwa hatua za kijeshi dhidi ya Iran.
Trump aliandika kwamba maseneta hao walituma ujumbe kwa Iran kwamba "hawajafurahishwa na hatua zangu dhidi yao na ni lazima nisitishe mapigano. Wamemsaidia adui."
Aliendelea kusema: ''Nilikuwa nimeiweka Iran chini ya shinikizo kali, walikuwa tayari kurudi nyuma, na walikuwa karibu kutupatia chochote. Kwa mara ya kwanza katika miongo kadhaa, Iran iliiheshimu sana Marekani na rais wake, (mimi). Lakini Bunge la Seneti la Marekani liliamua wakati mbaya zaidi, kupiga kura isiyo na maana ya Sheria ya Nguvu za Kivita,
Anasema Warepublican wanne walipiga kura na Democrats, na sasa Iran inawauliza wawakilishi wangu, 'Kura hii inamaanisha nini?'.
''Maseneta hawa wamefanya kazi yangu kuwa ngumu zaidi, lakini sitarudi nyuma, hata iweje, kwa sababu hivyo ndivyo ninavyofanya kazi kila wakati!".
Soma Zaidi: