Deni la taifa la Marekani lavuka dola trilioni 40
Takwimu kutoka Wizara ya Fedha ya Marekani zinaonyesha kuwa deni la taifa la Marekani limeongezeka maradufu ndani ya muongo mmoja, na kufikia dola trilioni 40.
Ongezeko hilo linatokana na miaka kadhaa ya matumizi makubwa chini ya uongozi wa marais Donald Trump na Joe Biden, pamoja na kupanda kwa viwango vya riba ambavyo vimeendelea kuongeza jumla ya deni hilo.
Mnamo mwaka wa 2016, deni la taifa la Marekani lilikuwa chini ya dola trilioni 20.
Ofisi ya Bajeti ya Bunge ilikuwa imekadiria kuwa jumla ya deni hilo ingefikia dola trilioni 39.6 kufikia mwisho wa mwaka wa fedha wa 2026.
Ongezeko hilo la kasi kuliko ilivyotarajiwa limezua wasiwasi kuhusu kasi ya ongezeko la mahitaji ya serikali ya Marekani ya kukopa fedha na athari zake kwa ongezeko la viwango vya riba hapo baadaye.
Ofisi ya Bajeti ya Bunge inasema kuwa Marekani inakaribia dola trilioni 1.41 na inatarajiwa kufikia takriban dola trilioni 64 kufikia mwaka wa 2036.
Wakati serikali ya Marekani ikitumia fedha zaidi kuziba pengo la bajeti yake, walaji wamejikuta wakikabiliwa na viwango vya juu vya riba na mfumuko wa bei.