Jinsi vita vilivyosababisha kuahirishwa kwa mazishi ya Khamenei

Chanzo cha picha, Reuters
Kutokana na vita kuendelea kupamba moto, maafisa wa Iran waliokuwa wakipanga mazishi ya mwezi Machi waliamua kuyaahirisha kabisa.
Wakati huo, afisa mmoja alisema kulikuwa na maombi mengi kutoka kwa watu waliotaka kuhudhuria hafla hiyo ya siku tatu katika ukumbi wa sala ulioko Tehran, na kwamba maandalizi ya miundombinu yalihitajika ili kupokea umati huo.
Khamenei aliuawa katika makazi yake mjini Tehran katika wimbi la kwanza la mashambulizi ya anga yaliyofanywa na Marekani na Israel, pamoja na mkwe wake wa kike, mjukuu wake wa mwaka mmoja aitwaye Zahra Mohammadi Golpayegani, na maafisa kadhaa waandamizi.
Mke wake pia iliripotiwa kuwa aliuawa katika shambulio hilo, ingawa baadaye chombo kimoja cha habari nchini Iran kilidai kuwa bado yuko hai.
Shughuli ya mazishi ya kiongozi huyo wa kidini mwenye umri wa miaka 86 ilikuwa imepangwa kufanyika tarehe 4 Machi, ambapo waombolezaji walitarajiwa kutoa heshima zao huku mwili wake ukiwa umehifadhiwa katika Msikiti Mkuu wa Grand Mosalla ulioko mji mkuu, Tehran.
Seyyed Mohsen Mahmoudi, mkuu wa Baraza la Uratibu wa Uenezi wa Kiislamu la Tehran, alisema kuahirishwa kwa mazishi hayo kulitokana na "idadi kubwa ya maombi ya kuhudhuria hafla hii na haja ya kuhakikisha maandalizi yanayofaa kwa ajili ya kuwahudumia wananchi."
Unaweza kusoma;























