Nairobi kuwa mwenyeji wa mkutano wa Africa Foward Summit 2026

Chanzo cha picha, Getty Images
Kenya inatarajiwa kuwa mwenyeji wa kongamano la kimataifa la Africa Forwad Summit 2026.
Mkutano huu utawaleta pamoja zaidi ya viongozi wa kitaifa 30,wawakilishi 4,000, wanabiashara mashuhuri 2,500, wawekazaji, mashirika yasiyo ya kiserikali na washirika wengine kutoka bara Afrika na jumuiya ya kimataifa.
Mkutano huo wa siku mbili utakao ongozwa na Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron na Rais wa Kenya William Ruto utafanyika katika ukumbi wa KICC jijini Nairobi.
Mkutano huu unatarajiwa kuimarisha uhusiano wa Ufaransa na Afrika katika sekta ya uwekezaji na uvumbuzi mbalimbali.
Marais mbali mbali ikiwemo rais wa Sierra Leone Julius Maada Bio, tayari wamewasili jijini Nairobi, huku usalama ukiimarishwa katika mji huo mkuu wa Kenya.
Barabara kuu za mji huo pia zinatarajiwa kufungwa siku ya Jumatatu na Jumanne.
Pia unaweza kusoma:






