Moja kwa moja, Hamas yakubali kuweka silaha chini Gaza; Trump kutangaza mpango wa Bodi ya Amani

Afisa mwandamizi wa Hamas ameliambia shirika la habari la BBC kwamba kundi hilo limekubali mpango wa Bodi ya Amani wa kuweka silaha chini kabisa katika Ukanda wa Gaza.

Muhtasari

Ruka Video uendelee
  • Besigye
  • .
  • xx
  • xx
  • xx
  • Lungu
  • xx
  • xx
  • d
  • s
  • a
  • Sonko
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • Dangote
  • xx
  • Lydia Wanjiku

Moja kwa moja

Na Asha Juma

  1. UEFA yatishia kususia Kombe la Dunia iwapo mipango ya FIFA itaidhinishwa

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Mpango wenye utata wa FIFA wa kuuza hisa katika mashindano yake kwa wawekezaji binafsi umepata pigo kubwa. Mashirikisho 41 ya soka kutoka Amerika Kaskazini, Amerika ya Kati na Caribbean yameukataa mpango huo, yakijiunga na upinzani wa pamoja wa mashirikisho yote ya Ulaya.

    Rais wa FIFA, Gianni Infantino, anasisitiza kuwa mpango huo ungeongeza kwa kiasi kikubwa ufadhili kwa mashirikisho ya soka ya kitaifa duniani kote.

    Mataifa yote 55 ya soka ya Ulaya yamekubaliana kususia Kombe la Dunia iwapo FIFA itatekeleza mpango huo. UEFA imesema timu zake zitashiriki katika mashindano ya FIFA tu iwapo mpango huo hautatekelezwa.

    Uamuzi huo ulifikiwa katika mkutano wa dharura wa Shirikisho la Soka la Ulaya (UEFA). Laura McAllister ni makamu wa rais wa Shirkisho la Soka Barani Ulaya.

    "Hatua ni wazi kabisa ni kitisho kwa mchezo wa soka kwa sababu pale tu utakapouza hisa kwa wawekezaji binafsi kwenye mpira ni wazi kabisa inatoa picha tofauti kabisa na msukumo wa tofauti kwa wale ambao ni ni wasimamizi wa Mchezo husika" alisema Laura.

    Uwezekano wa timu za Ulaya kujiondoa katika mashindano ya FIFA huenda ukawakatisha tamaa wawekezaji wa mradi huo wa kuuza hisa katika mashindano yake kwa wawekezaji binafsi chini ya Rais wake Gian Infantino, kwa kuwa timu za Ulaya ndizo zinazotawala mchezo wa soka.

    Soma Zaidi:

  2. Kenya yawa timu ya kwanza kuyaaga mashindano WAFCON 2026

    .

    Chanzo cha picha, CAF

    Fainali za Mataifa ya Afrika kwa wanawake zinaendelea nchini Morocco.

    Kenya imekuwa timu ya kwanza kuyaaga mashindano hayo baada ya kukubali kichapo cha goli 1-0 mbele ya Senegal.

    Kenya imetolewa kwa kufungwa michezo yote miwili ya mwanzo kwani katika mchezo wa kwanza ilichezea kichapo cha 4-0 mbele ya wenyeji Morocco.

    .

    Chanzo cha picha, CECAFA

    Katika mchezo mwingine wa kundi A, Morocco wamewachapa Algeria 1-0 na kufuzu kwa hatua ya robo fainali.

    Leo ni michezo miwili ya kundi B ambapo Ivory Coast inakipiga na Afrika Kusini kabla ya Tanzania kushuka dimbani dhidi ya Burkina Faso.

    Pia unaweza kusoma:

  3. Rais wa Kenya azungumzia mustakabali wa nchi baada ya mwaka 2030

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Rais wa Kenya, William Ruto, amesema atazindua rasmi mashauriano ya kitaifa tarehe 12 Agosti 2026 ili kujadili mustakabali wa nchi baada ya mwaka 2030.

    Katika hotuba yake iliyorushwa moja kwa moja kwenye televisheni siku ya Alhamisi, Rais alisema kuwa mjadala huo, aliouelezea kuwa tafakuri muhimu zaidi tangu kupitishwa kwa Katiba ya mwaka 2010, utahusisha serikali, vyama vya siasa, serikali za kaunti, wafanyabiashara na hasa vijana.

    Alisema Kenya inaweza kuwa nchi yenye ustawi mkubwa, mapato ya juu na ushindani wa kimataifa ndani ya kizazi kimoja, iwapo itaendelea kudumisha utulivu na umoja wa kitaifa.

    Rais Ruto aliahidi kuwaunganisha Wakenya wote, akisema kuwa mkataba wa maendeleo wa taifa “lazima uundwe na Wakenya wenyewe kupitia mazungumzo ya wazi na ushirikishi wa kitaifa.”

    “Haya si mazungumzo ya kuandaa waraka mwingine wa serikali. Ni kuhusu kujenga mwafaka mpya wa kitaifa,” alisema rais.

    Rais alikiri kuwa maono ya taifa baada ya mwaka 2030 yaani (Vision 2030), ambayo yalilenga kuifanya Kenya kuwa taifa la kipato cha juu cha kati ifikapo mwaka 2030, hadi sasa hayajafanikiwa kufikia malengo yake.

    Hata hivyo, alisisitiza kuwa serikali yake imefanikiwa kurejesha utulivu wa uchumi mkuu, kupunguza mfumuko wa bei pamoja na gharama za ukopaji, na kuimarisha akiba ya fedha za kigeni.

    Hotuba ya Rais Ruto, ambayo ilijikita zaidi katika maendeleo ya muda mrefu, haikutoa uzito mkubwa kwa changamoto za sasa kama vile deni la taifa, gharama kubwa ya maisha, ukosefu wa ajira kwa vijana, na ukatili wa polisi.

    Kenya itafanya uchaguzi mkuu mwezi Agosti 2027, na rais analenga kugombea muhula wake wa pili na wa mwisho wa miaka mitano kama rais wa nchi.

  4. Hamas yakubali kuweka silaha chini Gaza; Trump kutangaza mpango wa Bodi ya Amani

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Afisa mwandamizi wa Hamas ameliambia shirika la habari la BBC kwamba kundi hilo limekubali mpango wa Bodi ya Amani wa kuachana kabisa na silaha katika Ukanda wa Gaza huku akiongeza kuwa taarifa rasmi itatolewa hivi karibuni.

    Trump atangaza mpango wa Bodi ya Amani

    .

    Chanzo cha picha, EPA

    Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa Bodi ya Amani imefikia makubaliano ya kuhakikisha Hamas na makundi mengine yenye silaha katika Ukanda wa Gaza yanaweka silaha chini kabisa.

    Afisa mwandamizi wa Hamas ameliambia shirika la habari la BBC kwamba kundi hilo limekubali mpango wa Bodi ya Amani wa kuachana kabisa na silaha huko Gaza, na kwamba taarifa rasmi itatolewa hivi karibuni.

    Kwa upande wake, Israel bado haijatoa maoni au kauli rasmi kuhusu tangazo hilo.

    Trump amesema kuwa Israel itaondoka katika Ukanda wa Gaza kadri zoezi la kuachana na silaha litakapokamilika, na akayataja makubaliano hayo kuwa "hatua muhimu kuelekea Gaza hatimaye kutawaliwa na serikali mpya ya Kipalestina."

    Awamu ya pili ya mpango wa usitishaji mapigano huko Gaza ulioratibiwa na Marekani inajumuisha kundi la Hamas kuachana kabisa na serikali.

    Awamu hiyo ya pili pia inahusisha ujenzi upya wa Ukanda wa Gaza, ambao umeathiriwa vibaya na vita vya muda mrefu.

    Soma Zaidi:

  5. Hujambo msomaji wetu. Karibu katika matangazo ya moja kwa moja ya tarehe 31/07/2026