Tetesi za Soka Jumanne: Chiesa kuondoka Liverpool
Mshambuliaji wa Liverpool, Federico Chiesa, mwenye umri wa miaka 26, huenda akaondoka klabuni hapo Januari iwapo atakosa muda wa kutosha wa kucheza baada ya kurejea kutoka kwenye majeraha.. (Football Insider), external
Winga wa zamani wa Manchester United, Jadon Sancho, yuko kwenye mazungumzo na angalau klabu mbili za Ligi Kuu ya England kuhusu uwezekano wa kujiunga nazo.(Teamtalk)
AC Milan inapanga kumsajili kwa mkopo mshambuliaji wa Brazil, Endrick, mwenye umri wa miaka 20, kutoka Real Madrid mwezi Januari. (Calciomercato, external)
Manchester United bado inamtaka kiungo wa Leicester City, Louis Page, mwenye umri wa miaka 18, baada ya kushindwa kumsajili siku ya mwisho ya dirisha la usajili. (ESPN, external)
Manchester City inaendelea kumfuatilia kiungo wa Atletico Madrid, Alex Baena, mwenye umri wa miaka 25, ingawa huenda klabu hiyo isifanye uhamisho wake Januari. (Football Insider)
Liverpool na Manchester United zimewasiliana moja kwa moja na Wolves kuhusu uwezekano wa kumsajili winga mwenye umri wa miaka 18, Matheus Mane.(Ekrem Konur}
Brentford imeanza mazungumzo ya kuongeza mkataba wa mshambuliaji wake Mjerumani, Kevin Schade, mwenye umri wa miaka 24, katika jitihada za kuzuia Arsenal kumnasa.(Teamtalk)
Manchester United imekamilisha usajili wa kiungo wa Liverpool mwenye umri wa miaka 16, Isaac Konde.(Fabrizio Romano)
Soma Pia: