Hispania yafuzu fainali baada ya kuichapa Ufaransa

Chanzo cha picha, Getty Images
Beki wa Hispania na mchezaji bora wa mechi, Pedro Porro, amesema kufuzu kwa timu yake ni ndoto aliyokuwa akiisubiri kwa muda mrefu.
"Hii ni ndoto iliyotimia kwangu. Ilikuwa ndoto yangu kubwa zaidi. Nina furaha sana kwa timu. Tulicheza vizuri kuanzia mwanzo hadi mwisho na leo tulifanya kila tulichoweza ili kufuzu," alisema Porro.
Akizungumzia ushindi dhidi ya Ufaransa, Porro alisema walijua wangekutana na mpinzani mgumu lakini walitekeleza mpango wao ipasavyo.
"Tulijua tunakutana na timu ngumu sana. Huu ni ushindi wa timu nzima, si wangu pekee. Nawapongeza wachezaji wote kwa kiwango walichoonyesha."
Kuhusu jinsi walivyowadhibiti Wafaransa, Porro alisema umiliki wa mpira ulikuwa sehemu muhimu ya mkakati wao.
"Tulijua kumiliki mpira kungetusogeza karibu na ushindi. Mashambulizi yao ya kushtukiza ndiyo silaha yao kubwa, na kuyazuia ilikuwa jambo muhimu."
Porro pia alisema alitolewa uwanjani baada ya kuhisi hangeweza kuendelea kuchangia zaidi, akisisitiza kuwa ushindi huo ulitokana na mchango wa kikosi kizima.
"Nilihisi siwezi kuchangia zaidi. Ushindi huu umeletwa na wachezaji wote 26. Sasa tunaelekeza nguvu zetu kwenye fainali."
Alimalizia kwa kusema kuwa licha ya uchovu, Hispania itajipanga upya na kupambana kwa nguvu zote katika mchezo wa fainali.
Soma Zaidi:



