Serikali ya Tanzania
imepinga madai yaliotolewa na mgombea wa urais wa Zambia Brian Mandubile kwamba Tanzania ilituma watu kwenda kuingilia
uchaguzi mkuu wa taifa hilo uliofanyika hivi karibuni.
Mgombea huyo wa urais wa Zambia, aliwaonya Watanzania
anaodai wamehusika katika siasa za Zambia, akiwataka kuondoka nchini humo.
Lakini katika
taarifa iliotumwa katika mitandao ya kijamii, Tanzania imejibu kupitia barua
kwa ubalozi wake nchini Zambia ikitaka maelezo ya kina kuhusu sababu za mgombea
huyo kuzua madai kama hayo.
Tanzania
imesena inachukulia tuhuma hizo kwa uzito na kwamba inawahakikishia Watanzania na jamii ya kimataifa kwamba
haijatuma mtu yeyote Zambia kuvuruga uchaguzi wa taifa hilo.
‘’Kama
ilivyo nchi zingine za Jumuiya ya Maendeleo , kusini mwa Afrika SADC, Tanzania inao
uwakilishi wa waangalizi wa uchaguzi nchini Zambia wanaofanya kazi kulingana na
miongozo ya waangalizi wa uchaguzi wa SADC sambamba na waangalizi wengine
waliopo Zambia na sio kuingilia Uchaguzi kama ilivyotuhumiwa na bwana Mandubile’’.
Bwana
Mandubile alinukuliwa akisema kwamba
Zambia si
Tanzania na kwamba mbinu za kisiasa zinazoweza kufanya kazi Tanzania haziwezi
kutumika nchini Zambia.
Alisema: "Ndugu
zangu Watanzania ambao mmekodiwa, tafadhali tokeni katika nchi yetu."
Alisema
chama tawala cha UPND hakiwezi kushinda uchaguzi huo na kukituhumu kutumia kile
alichokiita "mbinu ya Tanzania" ili kupata ushindi.
"UPND
hawawezi kushinda uchaguzi huu, hakuna muujiza. Sasa wameamua kutumia mbinu ya
Tanzania. Zambia si Tanzania. Hii ni Zambia. Wale wanaofikiri wanaweza kuingiza
katika nchi hii mbinu inayofanya kazi Tanzania, hawawezi kufanikiwa
kamwe."
Kauli ya
Mundubile imekuja wakati mchakato wa kuhesabu kura katika uchaguzi wa Zambia
ukiendelea chini ya ulinzi mkali, baada ya Tume ya Uchaguzi ya Zambia
kusimamisha kwa muda zoezi hilo kufuatia taarifa za mashambulizi dhidi ya
maafisa wa uchaguzi na kuibwa kwa kura.
Tume hiyo
imesisitiza kuwa wagombea hawapaswi kujitangaza washindi kabla ya matokeo rasmi
kutangazwa.
Mundubile,
ambaye ni mmoja wa wagombea wakuu wa upinzani, tayari amejitangaza mshindi wa
uchaguzi huo, licha ya Tume ya Uchaguzi ya Zambia kutokuwa imetangaza matokeo
ya mwisho.