Kombe la Dunia: Ivory Coast yaaga, Afrika yasalia na timu saba

Chanzo cha picha, Getty Images
Ivory Coast imekuwa timu ya pili ya Afrika kuondolewa katika hatua ya 32 bora ya Kombe la Dunia baada ya kufungwa mabao 2-1 na Norway, na kuziacha timu saba za bara hilo zikiendelea na harakati za kutinga hatua ya 16 bora.
Kuondolewa kwa Ivory Coast kunaiunganisha na Afrika Kusini, ambayo iliaga hatua hiyo mapema, huku Tunisia ikiwa ilitolewa katika hatua ya makundi.
Katika mechi nyingine zilizochezwa usiku wa kuamkia leo, Ufaransa ilitinga hatua ya 16 bora baada ya kuichapa Sweden mabao 3-0, wakati Mexico nayo ilifuzu kwa kuishinda Ecuador mabao 2-0, asubuhi hii.
Sasa matumaini ya Afrika yapo kwa timu saba zilizobaki kwenye mashindano hayo.
Usiku wa leo saa moja usiku, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) itavaana na England, huku saa tano usiku Senegal ikikabiliana na Ubelgiji kuwania nafasi ya kutinga hatua ya 16 bora.
Ratiba ya Ijumaa inaonyesha Algeria ikicheza dhidi ya Uswisi, wakati Misri itavaana na Australia.
Maelezo zaidi:

















