Wafanyakazi wawili wafariki baada ya helikopta za kuzima moto kugongana nchini Ugiriki.
Wafanyakazi wawili wamefariki dunia baada ya helikopta mbili kugongana angani nchini Ugiriki wakati zikishiriki kuzima moto wa nyika.
Waliofariki ni rubani wa Denmark na afisa wa mawasiliano wa idara ya zimamoto ya Ugiriki. Rubani raia wa Uingereza na mratibu mwingine raia wa Ugiriki waliokuwa kwenye helikopta ya pili walinusurika.
Video ya tukio hilo, lililotokea takribani umbali 65 (mail42) magharibi mwa mji mkuu wa Athens, inaonesha helikopta aina ya Bell ikigonga mbawa za helikopta nyingine, ambayo ilishika moto. Helikopta nyingine ilitua kwa dharura.
Moto wa nchi umezuka nchini Ugiriki wiki hii na kusababisha uhamishaji wa watu kwa wingi. Nchi nyingine za Ulaya pia zimekumbwa na moto mkubwa na hatari wakati wa vipindi virefu vya joto kali.
Kwa mujibu wa Idara ya Zimamoto ya Ugiriki, helikopta hizo aina mbili za Bell—ambazo zimekodishwa kutoka kampuni ya Australia ya McDermott Aviation—ziligongana Jumapili wakati zikishiriki juhudi za kuzima moto mkubwa uliokuwa ukiwaka katika mpaka wa Attica na Boeotia.
Wafanyakazi wa helikopta moja waliokolewa wakiwa hai, huku wa helikopta ya pili wakipatikana wakiwa hawajitambui na baadaye kuthibitishwa kufariki dunia.
Waziri Mkuu wa Ugiriki, Kyriakos Mitsotakis, alielezea "masikitiko yake makubwa" kufuatia ajali hiyo.
Katika ujumbe kwenye mtandao wa X, alisema kupotea kwa mratibu huyo raia wa Ugiriki na rubani raia wa Denmark "kunatujaza sote huzuni." Pia alitoa rambirambi kwa familia zao.