Uingereza imesemema iko tayari kujilinda baada ya Iran kusema kuwa kambi zake ni ‘maeneo halali' kushambuliwa

Chanzo cha picha, EPA
Serikali ya Uingereza imesema iko tayari kujilinda saa 24 kwa siku, baada ya Iran kutangaza kuwa kambi za kijeshi za Uingereza zinazotumiwa na Marekani ni malengo halali ya kushambuliwa.
Uingereza imeiruhusu Marekani kutumia vituo vya kijeshi vya Uingereza vinavyohifadhi wanajeshi na ndege za Marekani kwa shughuli ilizozieleza kuwa za kujilinda, huku ikikataa kushiriki katika mashambulizi ya moja kwa moja dhidi ya Iran.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imeituhumu Uingereza kuwa mshirika wa Marekani katika vita hivyo, huku Kikosi cha Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) kikisema kuwa nchi yoyote itakayoiunga mkono Marekani kijeshi itabeba matokeo ya hatua hizo.
Kauli hiyo imekuja wakati Marekani ikiendelea na usiku wa 13 mfululizo wa mashambulizi dhidi ya malengo mbalimbali nchini Iran.
Rais wa Marekani Donald Trump amekuwa akiikosoa serikali ya Uingereza na aliyekuwa Waziri Mkuu Sir Keir Starmer, akidai hawajaunga mkono vya kutosha kampeni ya kijeshi ya Marekani.
Hata hivyo, Iran imeendelea kuichukulia Uingereza kama sehemu ya operesheni hiyo ya kijeshi.
Mwezi Machi, wakati wa siku za mwanzo za vita vinavyoongozwa na Marekani na Israel dhidi ya Iran, Uingereza iliruhusu Marekani kutumia vituo vya kijeshi vya RAF Fairford na Diego Garcia kushambulia miundombinu ya kijeshi ya Iran iliyodaiwa kutumika kushambulia mataifa ya Ghuba na meli katika Mlango bahari wa Hormuz.
Kwa mujibu wa taarifa, sera hiyo imeendelea hata baada ya Andy Burnham kuwa Waziri Mkuu mpya wa Uingereza, kufuatia uamuzi wa kuongeza muda wa makubaliano hayo na Marekani.
Katika taarifa iliyochapishwa na shirika la habari la Tasnim, linalohusishwa na IRGC, kundi hilo lilidai kuwa ndege za Marekani ziliondoka katika kambi ya RAF Fairford siku mbili kabla kutekeleza mashambulizi dhidi ya Iran.
Unaweza kusoma;







