Harry Kane afanya mazungumzo ya kuongeza mkataba Bayern Munich

Chanzo cha picha, Getty Images
Nahodha wa England, Harry Kane, yuko katika mazungumzo na Bayern Munich kuhusu kuongeza mkataba wake na mabingwa hao wa Ujerumani.
Mkataba wa Kane unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu ujao, lakini Bayern Munich ina nia ya kumbakisha mshambuliaji huyo kwa muda mrefu zaidi.
Kane pia anafahamu kuwa uongozi wa klabu hiyo unataka asaini mkataba mpya, huku taarifa zikieleza kuwa makubaliano yanaweza kukamilika katika wiki zijazo.
Mshambuliaji huyo alijiunga na Bayern Munich mwaka 2023 akitokea Tottenham Hotspur kwa ada ya pauni milioni 86.
Tangu kuwasili kwake, Kane ameisaidia Bayern kutwaa mataji mawili ya Bundesliga na Kombe moja la Ujerumani.
Pia alikuwa na mchango mkubwa kwa England katika Kombe la Dunia, akifunga mabao sita, huku akiwa ameifungia Bayern Munich jumla ya mabao 146 katika mechi 134 tangu ajiunge na klabu hiyo.
Hata hivyo, ripoti zinaeleza kuwa Barcelona inaendelea kufuatilia hali yake, wakati baadhi ya klabu za Saudi Arabia zikisubiri fursa ya kumsajili pindi mkataba wake utakapomalizika.
Soma Zaidi:






















