Mfalme Charles afichua kuwa alilipa ushuru wa pauni milioni 12.9 mwaka 2024-25
Chanzo cha picha, Getty Images
Mfalme Charles amekuwa mfalme wa kwanza wa Uingereza kuweka adharani kiwango chaa kodi anacholipa.
Mfalme Charles Alilipa dola milioni 17 kutokana na mapato yake binafsi katika mwaka wa kodi ulioishia Machi, 2025.
Mfalme Charles amelipa takriban dola milioni arobaini kama kodi tangu alipokuwa Mfalme mnamo mwaka wa 2022.
Mwanafalme William, pia ameweka wazi maelezo yake ya kodi, William alilipa dola milioni 10 katika mwaka uliopita wa kodi.
Kando na hayo, imebainika kuwa Mfalme Charles na Malkia Camilla hawaishi tena katika Ikulu ya Buckingham Palace licha ya jengo hilo kufanyiwa ukarabati ambao tayari umegharimu dola za Marekani milioni 430 itakapokamilika mwaka ujao.
Badala yake, watasaliai katika jumba jirani la Clarence.
Wataendelea kutumia Kasri la Buckingham shughuli za kiserikali.
Kombe la Dunia 2026: Ivory Coast yafuzu raundi ya pili baada ya kuilaza Curacao
Chanzo cha picha, Getty Images
Maelezo ya picha, Nicolas Pepe
Ivory Coast imefuzu kwa hatua ya muondoano kwa mara ya kwanza katika historia ya Kombe la Dunia baada ya Nicolas Pepe kufunga mabao mawili na kuwaondoa Curacao.
Wenyeji Ivory Coast walihitaji alama moja tu ili kufika hatua ya 32, baada ya kutoka katika hatua ya makundi katika mechi zao tatu zilizopita za Kombe la Dunia.
Na walionyesha ujasiri wao kwa bao baada ya dakika saba tu mabeki wa Curacao walishikwa wavuni na kuondolewa na Yan Diomande, ambaye alimuandalia mpira safi Pepe.
Katika dakika ya 65, mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Pepe - ambaye aliachwa nje ya kikosi cha Ivory Coast kwa ajili ya Kombe la Mataifa ya Afrika mapema mwaka huu - alipata la pili alipopachika wavuni kwa mguu wa kushoto na kumpita kipa wa Curacao, Eloy Room.
Hii inamaanisha kuwa Ivory Coast inamaliza nafasi ya pili katika Kundi E ikiwa na alama sita, ikishinda mechi mbili za Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza.
Tetemeko la ardhi Venezuela: Waokoaji mbioni kuwatafuta manusura, idadi ya waliofariki ikifikia 235
Chanzo cha picha, Getty Images
Waokoaji wanapekua vifusi watafuta walionusurika matetemeko mawili makubwa ya ardhi yaliyokumba maeneo ya karibu na mji mkuu wa Venezuela na kusababisha vifo vya takribani watu 235 na kuwajeruhi zaidi ya 1,500.
Katika Caracas na mji wa karibu wa pwani wa La
Guaira, watu walisikika wakiomba msaada kutoka chini ya vifusi vya majengo
yaliyoporomoka.
Tetemeko la kwanza la ukubwa wa 7.2 lilifuatiwa
sekunde chache baadaye na lingine lenye nguvu zaidi ya 7.5, kulingana na
Utafiti wa Jiolojia wa Marekani (USGS), na kusababisha uharibifu mkubwa zaidi.
Watu wengi zaidi wanahofiwa kufariki, huku wengine
wakiwa wameachwa bila makao au kulala barabarani kwa kuogopa kurejea kwenye
majengo yaliyoharibiwa baada ya mkasa huo.
Matetemeko ya ardhi yalitokea saa kumi na mbili na
dakika ne kwa saa za ndani(22:04 GMT) siku ya Jumatano - sikukuu ya kitaifa
nchini Venezuela, kumaanisha kuwa watu walikuwa nyumbani ikilinganishwa na siku
ya kawaida ya juma.
Siku ya Alhamisi Rais wa Bunge la Venezuela Jorge
Rodríguez, aliripoti kwamba idadi ya waliofariki imeongezeka, baada ya Rais wa
mpito wa nchi hiyo Delcy Rodríguez kutangaza hali ya dharura.
Nchi kadhaa zimeahidi kusaidia juhudi za uokoaji,
huku Marekani ikiahidi msaada wa dola milioni 150. Jeshi la Marekani linatuma
meli za usafiri na ndege kusaidia shughuli ya uokoaji na "operesheni za msaada
wadharura", ilisema katika taarifa.
Jorge Rodríguez alisema majengo 250 yameharibiwa au
kupotea, hasa La Guaira, ambapo BBC ilithibitisha picha za hoteli ya ghorofa 10
iliyoharibiwa na kuwa vifusi. Siku ya Alhamisi, watu walikuwa wakitafuta
wapendwa huko.
Juan Ortiz ameiambia BBC kwamba mmoja wa marafiki
zake wa karibu amethibitishwa kufariki, mwingine anaaminika kuwa chini ya
vifusi, na takribani watu 20 anaowafahamu wanaoishi katika eneo la pwani hawajulikani
waliko.
"Ninakabiliwa na mshtuko na kuchanganyikiwa, nasikitika
kwamba siwezi kusaidia," mwanafunzi wa matibabu mjini Caracas alisema.
UN yasitisha mpango wa uokoaji wa Mlango wa Bahari wa Hormuz baada ya meli ya mizigo kushambuliwa
Chanzo cha picha, Reuters
Shirika la Umoja
wa Mataifa la Usafiri wa Baharini (IMO) limesitisha mpango wa kuwahamisha zaidi
ya mabaharia 11,000 waliokuwa wamekwama kwenye Mlango-Bahari wa Hormuz baada ya
meli ya mizigo iliyokuwa ikipita kwenye njia hiyo ya majini kushambuliwa.
Mkuu wa IMO
Arsenio Dominguez alisema boti kadhaa tayari zimeondolewa, lakini shirika hilo
lilitaka kuhakikisha kuwa "usalama" utaendelea
kudumishwa.
Shirika la
usalama wa baharini la Uingereza UKMTO liliripoti siku ya Alhamisi kuna meli ambayo imeshambuliwa kwa "kifaa kisichojulikana" maili 7.5 kusini-mashariki mwa bandari ya Dahit ya Oman. Hakuna majeruhi walioripotiwa.
Kampuni ya
usimamizi wa hatari za baharini ya Vanguard ilisema meli hiyo, yenye bendera ya
Singapore, Ever Lovely, iliendelea na safari licha ya shambulio hilo.
Maafisa wa
Marekani walisema Iran ilishambulia meli hiyo, kwa mujibu wa ripoti
za vyombo vya habari vya Marekani. Chombo kilichoundwa na Iran kusimamia mkondo
wa bahari kilisema meli zinazopita nje ya njia zilizotengwa hazitahakikishiwa usalama.
Katika chapisho
kwenye X, Mamlaka ya Mlango-Bahari ya Ghuba ya Uajemi (PGSA) ilisema:
"Madhara yoyote yanayotokana na utumiaji wa njia zisizoidhinishwa itakuwa
jukumu la mmiliki, mwendeshaji na bwana wa meli".
Mamia ya meli na
maelfu ya mabaharia wamekwama katika Ghuba tangu Februari kwa sababu ya vita vya
Marekani na Israel dhidi ya Iran.
Juhudi za
kuwahamisha Umoja wa Mataifa zilitangazwa Jumanne baada ya kufunguliwa tena
kwa mlango wa bahari huo, huku Dominguez akisema "operesheni hiyo
kubwa" ilikuwa na ushirikiano wa Iran, Oman, Marekani, mataifa mengine ya
pwani katika eneo hilo na sekta ya bahari.