Maambukizi 906 yanayoshukiwa kutokana na aina ya Bundibugyo ya Ebola - WHO
Shirika la Afya Duniani (WHO) linasema kuna visa 906 vinavyoshukiwa vya Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), ikiwa ni pamoja na vifo 223 vinavyoshukiwa ambavyo vinachunguzwa.
Mkuu wa Shirika la Afya Ulimwenguni anasafiri kuelekea katikati mwa mlipuko wa sasa wa Ebola - mkoa wa Ituri mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Tedros Adhanom Ghebreyesus anazuru nchi hiyo ili kuimarisha juhudi za kudhibiti kuenea kwa virusi hatari.
Ameonya kuwa kuna changamoto nyingi - kwa sababu ni virusi adimu na hadi kufikia sasa bado hakuna chanjo na eneo lenyewe linakabiliwa na migogoro na watu wengi kuhama makazi yao, na kuchangia kueneza ugonjwa huo.
WHO inasema uwezo wa kufanya vipimo umeimarika.
Mlipuko wa aina adimu ya virusi vya Bundibugyo mashariki mwa nchi hiyo unatishia kulemea mamlaka za afya, huku visa vikiripotiwa pia nchini Uganda.
Kumekuwa na visa 125 vilivyothibitishwa vya Ebola nchini DRC, ikiwa ni pamoja na vifo 17 vilivyothibitishwa huko Ituri, Kivu Kaskazini na Kivu Kusini, tangu mlipuko huo ulipoanza takriban miezi miwili iliyopita.
Pia kumekuwa na visa tisa vilivyothibitishwa vya Ebola nchini Uganda, karibia vitatu kati ya hivyo chanzo chake ni DRC, na kifo kimoja. Hata hivyo, hakuna maambukizi ya jamii yaliyoripotiwa, WHO ilisema.
Soma zaidi: