Mlango wa bahari wa Hormuz 'hautarejea' ulivyokuwa kabla ya vita - vyombo vya habari vya Iran

Chanzo cha picha, Getty Images
Chini ya makubaliano kati ya Marekani na Iran, Mlango wa bahari wa Hormuz "hautarejea katika hali yake ya kabla ya vita" linaripoti shirika la habari la Iran la Tasnim.
Chombo hicho cha habari kilicho na uhusiano na Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) kimekuwa kikiripoti maelezo yaliyomo kwenye makubaliano hayo na Marekani asubuhi hii, lakini Marekani haijathibitisha kuhusu maelezo ya makubaliano yoyote.
Tasnim inaripoti kwamba mlango huo wa bahari hautarudi katika "ilivyokuwa" lakini idadi ya meli zinazopita inaweza kurudi katika viwango vya kabla ya vita ndani ya siku 30.
Hata hivyo, inaongeza kuwa Iran "inasisitiza kutumia mamlaka yake kuhusu uamuzi huo".
Inaongeza kuwa kizuizi cha majini cha Marekani dhidi ya meli zinazoingia na kutoka bandari za Iran lazima "kiondolewa kabisa" ndani ya siku 30.
Maelezo zaidi:

